Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 86 2021-04-16

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDD K. IDDI aliuliza:-

Je, nili ni Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Geita – Bukoli hadi Kahama kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kasimu Iddi Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na maandalizi ya makabrasha ya zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Geita – Bukoli hadi Kahama yenye urefu wa kilomita 139 inayounganisha mikoa ya Geita na Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, kazi hii ilifanywa na Mhandisi Mshauri ENV Consult (T) Ltd kwa gharama ya Shilingi milioni
440. Kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Aidha, Kampuni ya Uchimbaji Madini BARRICK imeonyesha nia ya kufadhili ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Kahama – Bulyanhkulu – Geita yenye urefu wa kilometa 120.2. Kwa sasa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Wizara ya Madini zinaendelea na mazungumzo na Kampuni ya BARRICK Kuhusu utaratibu wa ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, wakati ujenzi wa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha Wizara yangu inaendelea kuihudumia barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka wa fedha huu wa 2020/2021, jumla ya shilingi milioni 872.966 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hiyo.

Aidha, ninapenda kulifahamisha Bunge lako tukufuku kuwa ili ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ufanyike, hatua mbalimbali hufuatwa ambazo ni pamoja na upembuzi yakinifu, usanifu wa kina. Utayarishaji wa Nyaraka za zabuni na taratibu za ununuzi za kumpata mkandarasi wa ujenzi. Hivyo, kukamilika kwa hatua tajwa, maana yake nikuanza kwa mradi husika. Ahsante.