Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaweka taa katika barabara kuu ya Mji wa Maswa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO Mheshimiwa Spika nashukuru kwa majibu ya Serikali, na niwapongeza Serikali kwa kuanza kufanya mradi huu kwa kuweka taa za barabara kuu za Mji wa Maswa. Ninachosikitika ni kwamba mradi huu umekwenda nusunusu sasa naomba Mheshimiwa anipe majibu ya kweli wameweka taa 18

Je, wana mpango wa kuweka taa ngapi ambazo zitatosha kuanzia Mwigumbi kwenda njia panda.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa Maswa wanapata shida barabara hiyo zinapopita gari kwa kasi kubwa watu wanapata ajali na wengine wanapoteza maisha na kuna mpango wa kutengeneza bypass road kuzunguka Mji wa Maswa.

Je, barabara hiyo nayo itajengwa lini? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba katika barabara zote za sasa ambazo zinatengenezwa imekuwa ni sehemu ya mkataba kwamba pale ambapo barabara zinapita kwenye Miji, moja ya eneo ambalo lazima lishughulikiwe na Wakandarasi ni kuweka taa za barabarani ikiwemo Mji wa Maswa. Taa sizopungua 60 zitaweka katika Mji wa Maswa ili kukamilisha Mji wote kwenye barabara ile kuu, swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, bypass road ya Maswa itajengwa kulingana na upatikanaji wa fedha ipo kwenye mpango na itajengwa mara tu Serikali itakapokuwa imepata fedha ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaweka taa katika barabara kuu ya Mji wa Maswa?

Supplementary Question 2

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika nashukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ya Maswa ina umuhimu sana sawasawa na barabara ya watu wa Kibiti kutoka Kibiti Dimani kwenda Mloka kule ambako kuna ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, na kwa kuwa Mheshimiwa Rais mama yetu Samia wakati anainadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi aliahidi kwamba barabara ile itajengwa kwa kiwango cha lami.

Je, ni lini Serikali itatenga fedha ili shughuli za awali za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zianze mara moja katika barabara hiyo? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Kibiti ni moja ya barabara muhimu sana ambayo ni moja ya njia inayofika kwenye Bwawa la Nyerere, na barabara hii ni ahadi ya viongozi wetu wa Kitaifa.

Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Kibiti, kwamba barabara hii ipo kwenye mpango na itajengwa kwa kiwango cha lami kama viongozi ambavyo wametoa ahadi na kama ambavyo inaonekana kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi ahsante.