Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 85 2021-04-16

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaweka taa katika barabara kuu ya Mji wa Maswa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, kama ifuatavyo:- Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) ilishaanza kazi ya uwekaji taa katika barabara kuu ya Mwigumbi hadi Maswa eneo la Maswa Mjini katika mwaka wa fedha 2020/2021. Jumla ya taa za barabarani 18 zimeshawekwa ambazo zimegharimu jumla ya Shilingi milioni 81.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini TANROADS, imepanga kuendelea na uwekaji wa taa katika barabara kuu katika Mji wa Maswa katika mwaka wa fedha 2021/2022. Ahsante.