Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VICENT P. MBOGO aliuliza:- Jimbo la Nkasi Kusini lina Kata 11 na Kituo cha Afya kimoja pekee:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vituo vya Afya hasa katika Tarafa ya Chala, Kate, Myula, Sintali na Ninde?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri. Ukanda wa Ziwa Tanganyika akina mama wengi wanakufa kwa kutokupata huduma za afya, hasa upande wa ambulance boat kwa sababu kule miundombinu ya barabara hakuna, usafiri wao ni ndani ya maji na vijiji vipo vingi sana ndani ya Ziwa Tanganyika ambavyo vinatumia usafiri wa boti. Ni lini Serikali itapeleka ambulance boat kwa ajili ya kuokoa akina mama wajawazito? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba katika mwambao ule wa Ziwa Tanganyika kuna changamoto ya usafiri pale ambapo tunapata dharura za wagonjwa na hususan akina mama wajawazito ambao wanahitaji kwenda kwenye vituo vya rufaa kwa ajili ya huduma za upasuaji. Serikali imeendelea kuweka mipango ya kuhakikisha kwamba maeneo hayo ambayo yana changamoto kubwa za usafiri, hasa ambulance kwa maana ya ambulance boats, tunaendelea kuangalia utaratibu mzuri zaidi wa kutenga fedha kadri zitakavyokuwa zinapatikana ili tuwezeshe ufanisi wa rufaa katika maeneo hayo ili tuendelee kuokoa maisha ya wananchi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo kwamba suala hili kama Serikali tunalichukua, tutalifanyia kazi na kuona namna bora zaidi ya kupata ambulance boat ili iweze kusaidia wananchi katika Jimbo la Nkasi Kusini. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. VICENT P. MBOGO aliuliza:- Jimbo la Nkasi Kusini lina Kata 11 na Kituo cha Afya kimoja pekee:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vituo vya Afya hasa katika Tarafa ya Chala, Kate, Myula, Sintali na Ninde?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Makete, hasa Kata za Ipepo na Ikuo, wana changamoto pia ya kituo cha afya. Kwa Ikuo wana majengo tayari wameshajenga kwa nguvu za wananchi lakini bado Serikali haijamalizia na Ipepo tayari wameshaandaa tofali kwa ajili ya kujenga kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itaongeza nguvu kuhakikisha kwamba majengo haya yanakamilika kwa ajili ya wananchi wangu wa Ipepo na Ikuo, hasa ikizingatiwa kwamba wana zaidi ya kilometa 20 kwenda kufuata huduma za afya na tayari wameshaonesha jitihada za kuweka nguvukazi hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu ya Serikali kwa ajili ya wananchi wangu hao.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kuwapongeza wananchi wa Kata za Ipepo na Ikuo katika Jimbo la Makete kwa kuonesha nguvu kubwa ya kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya afya na hatua nzuri ambayo wameifikia. Serikali imeendelea kusisitiza wananchi kuchangia nguvu zao kuanza ujenzi wa miradi ya vituo vya afya na zahanati na Serikali kuchangia nguvu za wananchi katika umaliziaji wa vituo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Festo Sanga kwamba katika mwaka ujao wa fedha, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuchangia nguvu za wananchi katika ukamilishaji wa maboma. Nimhakikishie kwamba katika maeneo ambayo tutawapa kipaumbele ni pamoja na Kata hizi za Ipepo na Ikuo ili wananchi waweze kupata nguvu ya Serikali kukamilisha vituo hivyo vya afya.

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. VICENT P. MBOGO aliuliza:- Jimbo la Nkasi Kusini lina Kata 11 na Kituo cha Afya kimoja pekee:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vituo vya Afya hasa katika Tarafa ya Chala, Kate, Myula, Sintali na Ninde?

Supplementary Question 3

MHE. HAMIS M. MWINJUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kwa Jimbo la Nkasi Kusini, hali ni hiyohiyo ama mbaya zaidi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza ambapo tuna kata 37 na vituo viwili tu vya afya. Sasa swali langu, Serikali ina mpango wowote wa kuongeza vituo vya afya Wilayani Muheza ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamis Mwinjuma, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Jimbo la Muheza lina kata 37 na vituo vya afya viwili tu na hali hii ipo katika karibu majimbo yote nchini. Tunafahamu tuna kata zaidi ya 3,900 na ndiyo maana Serikali imeweka mpango wa kujenga vituo vya afya kwa awamu. Ni kweli kwamba hatuwezi kukamilisha kujenga vituo katika kata zote ndani ya mwaka mmoja wa fedha, lakini Serikali imedhamiria na inatambua kwamba tuna kazi ya kufanya kwa awamu kwa kadri ya fedha zinavyopatikana na kuendelea kujenga vituo vya afya katika kata zetu na kujenga zahanati katika vijiji na hospitali za halmashauri katika ngazi za halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mwinjuma kwamba katika mipango ya Serikali inayokuja, tutaendelea kuomba kuidhinishiwa fedha kwa ajili ya kuendelea kujenga vituo vya afya katika kata nchini kote zikiwemo kata katika katika Jimbo hili la Muheza.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. VICENT P. MBOGO aliuliza:- Jimbo la Nkasi Kusini lina Kata 11 na Kituo cha Afya kimoja pekee:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Vituo vya Afya hasa katika Tarafa ya Chala, Kate, Myula, Sintali na Ninde?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Changamoto iliyopo Nkasi ndiyo changamoto iliyopo Kyerwa. Kyerwa tuna kata 24 lakini vituo vya afya vinavyotoa huduma ni viwili na kipo Kituo cha Afya Nkwenda ambacho jengo la mama na mtoto halijakamilika. Lini Serikali itakamilisha kituo hiki ili kiweze kutoa huduma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimetangulia kutoa ufafanuzi, kwamba dhamira na malengo ya Serikali na katika mipango yote ambayo Serikali inaandaa, ni pamoja na kuhakikisha inachangia nguvu za wananchi katika kukamilisha maboma ya zahanati, vituo vya afya na kupanua hospitali za halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo hili la Kyerwa ambapo kuna vituo vya afya viwili na Kituo cha Afya cha Nkwenda ambacho kimeshajengewa jengo la RCH na halijakamilika, ni miongoni mwa vituo ambavyo vitaendelea kupewa kipaumbele katika bajeti za Serikali ili viweze kukamilishwa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba katika mwaka ujao wa fedha, Mheshimiwa Waziri akija kuwasilisha bajeti hapa, tuna vituo takribani 121 ambavyo tunatarajia kwenda kujenga kwa fedha za Serikali Kuu na fedha za mapato ya ndani ya halmashauri. Kwa hiyo kwa kupitia mpango huo tutaendelea kusogeza zaidi huduma ikiwemo katika Jimbo hili la Kyerwa.