Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kinyata kwa njia nne kutoka Mwanza Jiji kuelekea Usagara?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na changamoto za kifedha kama ambavyo Mheshimiwa Waziri ameeleza lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo jibu la Waziri linasema ujenzi wa barabara hii baada ya Mkandarasi Mshauri kuwa amekamilisha kazi yake itategemea na upatikanaji wa fedha. Upatikanaji wa fedha ni kweli kwamba unaweza ukachukua hata zaidi ya miaka mitatu au minne. Swali langu la kwanza, kwa sababu barabara sasa hivi imekuwa na magari mengi takriban 2,000 kwa siku kutoka Nyegezi kwenda Usagara mpaka Mjini, Serikali itakuwa tayari angalau kuanza kwa hatua mbili; walau baada ya Mkandarasi Mshauri kumaliza itakuwa tayari kuanza kujenga hata kwa km 10 kwa phases na baadaye km 10?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, wako watu kutoka Kata ya Nyegezi na Mkolani ambao wameongezeka zaidi ya mita 7.5 kwenye barabara hii na watu hao wanastahili kulipwa fidia. Je, Serikali itakuwa tayari kuwalipa fidia stahiki kwa sababu za msingi ili barabara hii iweze kujengwa bila vikwazo na wananchi wapate huduma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, usanifu wa kina utakamilika Septemba na baada ya hapo barabara hiyo itaanzwa kujengwa kwa kiwango cha lami. Kuhusu upatikanaji wa fedha na ni kwa kiasi gani tunaweza kujenga, matarajio ya Serikali ni kukamilisha barabara lakini tutaanza kadri fedha itakavyopatikana ndiyo tutaanza kujenga kama ni km 5, km10 ama ikiwezekana zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu fidia, hatutajenga bila kufanya tathmini na ndiyo maana ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao unachukua masuala yote; kuangalia ni kiasi gani cha fedha kinatakiwa ili wananchi wa Kata za Buhongwa na Nyegezi ambao wameongezeka sana watafidiwa. Ni utaratibu kwamba ni pale ambapo wananchi wa Kata za Buhongwa na Mkolani watakapokuwa wamefidiwa ndipo ujenzi utaanza. Ahsante.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kinyata kwa njia nne kutoka Mwanza Jiji kuelekea Usagara?

Supplementary Question 2

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika Bunge lililopita la Kumi na Moja, Bunge lako Tukufu lilielezwa kwamba Serikali imetenga shilingi bilioni 5 kuanza kuweka lami barabara ya kutoka Same Kisiwani - Mkomazi. Je, kazi hii itaanza lini? Ahsante (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naghenjwa Kaboyoka, Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama Serikali ilivyoahidi kwamba imetenga shilingi bilioni tano kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Same Kisiwani, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba bado barabara nyingi hazijatangazwa na zitaendelea kutangazwa kadri tunavyokwenda na barabara nyingi tu zitatangazwa kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha. Pia tunategemea baada ya bajeti hii barabara hizo zitaendelea kujengwa ikiwa pengine ni pamoja na hii Same Kisiwani, itategemea na bajeti hii tunayoendelea kuipitisha itakavyokuwa imepita. Ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kinyata kwa njia nne kutoka Mwanza Jiji kuelekea Usagara?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati DKt. John Pombe Magufuli, alivyokuwa Karagwe aliahidi kwamba watu wa Kyerwa watajengewa barabara kilomita 50 kwa lami. Hii barabara ya lami inahitajika kweli kwa sababu imekuwa ni mgogoro wa wananchi, je, itaanzia wapi hiyo kilomita 50 ya lami? Licha ya kuahidiwa bado ujenzi huo haujaanza. Swali, ni lini hizo kilometa 50 tulizoahidiwa na Mheshimiwa Rais zitaanza kujengwa hata ikibidi tukaongezewa zikawa hata 100? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ahadi zote za Viongozi wa Kitaifa tunazizingatia na huwa tunazitekeleza. Ahadi ikishatolewa kuanza kwa barabara si kuingia site na kuona magreda yanaanza kutembea lakini barabara itafanyiwa usanifu na usanifu wa kina ndipo itakapoanza kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la pili barabara itaanzia kujengwa wapi, sisi kama Serikali kokote tukianzia ili mradi kilomita 50 zitatimia tutaijenga barabara hiyo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea na taratibu za kutimiza ahadi za Viongozi wa Kitaifa ikiwa ni pamoja na barabara hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja kwamba zitajengwa kama zilivyoahidiwa na Kiongozi wetu wa Kitaifa. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kinyata kwa njia nne kutoka Mwanza Jiji kuelekea Usagara?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Umuhimu wa barabara ya Kenyatta katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza ni sawa kabisa na umuhimu wa barabara ya kutoka Kiranjeranje - Nanjilinji mpaka Ruangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Jimbo la Kilwa Kusini. Lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii ni kati ya barabara ambazo zimeainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ni barabara ambayo pia imeahidiwa na viongozi wa Kitaifa. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kadri fedha itakapopatikana barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami mara baada ya kukamilisha usanifu wa kina wa barabara hii. Ahsante.