Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 56 2021-04-12

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Kinyata kwa njia nne kutoka Mwanza Jiji kuelekea Usagara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nyamagana – Usagara ni sehemu ya barabara Kuu ya Mwanza – Shinyanga Mpakani yenye urefu wa kilometa 104. Barabara hii ni muhimu katika kukuza uchumi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na ni kiunganishi kati ya Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na nchi jirani.

Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeanza mipango ya kuanza ujenzi wa barabara ya Mwanza hadi Usagara kwa njia nne. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii unaendelea ambapo umezingatia kupanua barabara hii kuwa na njia nne kuanzia Mwanza Mjini hadi Usagara yenye urefu wa km 22. Kazi hii inafanywa na Mhandisi Mshauri M/s NIMETA Consult (T) Ltd ya Tanzania kwa gharama ya Shilingi Milioni 980.84. Aidha, usanifu wa kina unatarajiwa kukamilika Septemba, 2021 na baada ya kukamilika barabara hiyo itaingizwa kwenye mpango wa ujenzi ikiwa ni pamoja na upanuzi wa njia hizo nne kutoka Mwanza Jiji hadi Usagara kutegemea na upatikanaji wa fedha. Ahsante.