Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na wa kazi wa Mtaa wa Kinyambi na Bugosi katika Halmashauri ya Mji wa Tarime?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini ningependa kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mtaa wa Kinyambi na Bugosi hawafanyi shughuli zozote katika maeneo yale, na wengi wao walikuwa wanafanya shughuli ndogo ndogo za kujikimu kama kilimo na shughuli zingine na ukizingatia kwamba ni muda mrefu sasa tangu uthamini ufanyike, mwaka 2013 hadi sasa.

Je, wale wananchi wanaweza kuruhusiwa kuendelea na shughuli zile ili waendelee kujikimu badala ya kutaabika na kuendelea kukaa pale bila kufanya shughuli ambazo zinawaongezea kipato? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu kwamba maeneo yote ambayo yanamilikiwa na Jeshi letu ni muhimu na kwa manufaa ya nchi yetu na kwa wananchi kwa ujumla. Lakini niseme tu kwamba uwepo wa maeneo haya umepangwa kistratejia (strategically), tumejipanga kwa ajili ya kuhakikisha kwamba kazi za jeshi zinafanyika vizuri. Niwaombe tu wananchi waweze kuvuta subira; kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunafanyia kazi ili tuweze kuwatendea haki wananchi hawa; hii ni pamoja na kuwalipa fidia zao ambazo zitawawezesha kwenda kufanya shughuli zao zingine.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge kwanza nikupongeze kwa namna ambavyo mara kadhaa tumeweza kuzungumza na Mbunge ili tuone namna nzuri. Kikubwa nachoweza kusema hapa ni kwamba sisi tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba zoezi hili linakamilika mapema na wanachi wanapata haki zao. Tunaogopa kwamba tukiwaruhusu wananchi wakiendelea kutumia maeneo haya wanaweza wakafanya vitu ambavyo vina gharama kubwa na baadaye vikawatia hasara ndugu zetu hawa wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wavute subira tu, nafikiri tutaendelea kushughulikia suala hili kwa kuwasiliana Serikali zetu za Wilaya na Mkoa ili tuone namna nzuri ya kuwafanya wananachi wasikwame, waendelee kufanya uzalishaji na shughuli zao zingine. Ahsante sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na wa kazi wa Mtaa wa Kinyambi na Bugosi katika Halmashauri ya Mji wa Tarime?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru ni dhahiri kwamba maeneo ya Bugosi na Kinyambi ni tatizo la takriban miaka 17. Mara ya mwisho Serikali kupitia aliyekuwa Waziri wa Ulinzi ambaye ni Rais wa Zanzibar kwa sasa walifanya tathimini kwa mara ya pili hapo mwaka jana na wakawa wameshajiridhisha kwamba ile ya kwanza ilikuwa inawapunja Watanzania wale wa Tarime, na wakasema tayari wameshapitisha wanasubiri HAZINA kulipa hela na aliyekuwa Waziri wa Fedha ambaye ni Makamu wa Rais alidhihirisha hili kwamba tayari Fedha za Tarime zipo tayari kulipwa.

Mheshimiwa Spika, sasa hayo wanayokuja kusema leo inaonyesha ni jinsi gani Serikali haitoi umakini na uzito pale ambapo wananchi wamekuwa wametwaliwa ardhi. Sasa, ningeomba Mheshimiwa Waziri alete zile fedha ambazo zilishapitishwa tayari walikuwa wanasubiria Hazina kutoa ziende kuwalipa wale wananchi wa Tarime ili waende maeneo mengine wapishe jeshi lifanye shughuli zao. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Matiko kama ifuatavyo:-

Mheshimwa Spika, niseme tu kwamba ule umakini wa kuhakikisha kwamba wananachi wanapata haki yao ndio huo ambao kwa namna nyingine umesababisha tumechelewa. Pia tumechelewa kwa sababu yapo matatizo kadhaa, Mheshimiwa Matiko anafahamu. Kwamba wakati wa zoezi hili likifanyika kwenye uthamini, na kwa uzoefu umeonyesha maeneo mengi, kumekuwa na changamoto hizi, na hasa Serikali inapoona kwamba kuna wananchi watakosa haki zao.

Mheshimiwa Spika, ni muhimu sana tukazingatia kwamba wananchi wapate haki zao. ndiyo maana unaona hata uthamini uliochelewa kwa utaratibu wa sheria na kanuni zilizokuwepo kwa nia hiyo hiyo ya kuwa-compensate wananchi kile ambacho wamechelewa kukipata ndiyo maana tunafanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge, vuta Subira; na sisi tumejipanga na sasa tunacho kitengo cha milki kwa nia ya kuhakikisha kwamba kinafanya kazi yake vizuri kwa matatizo hayo. Yako matatizo mengi maeneo mbalimbali; kwamba tumeweka kitengo hiki ili kiweze ku-coordinate ili tuone zile changamoto ambazo zilikuwa zinatokea zinaondoka. Tukienda kwenye hatua ya uhakiki wenzetu upande wa Hazina na kadhalika; changamoto nyingi zimekuwa zikionekana lakini tumedhamiria kuona kwamba maeneo haya,maeneo ya Tarime na maeneo mengine nchini yako mengi tunafanya hivyo kuhakikisha kwamba ile migogoro iliyokuwepo tunaenda kuimaliza. Kwa hiyo Mheshimiwa Matiko naomba uvute subira na ninaamini kwamba tutaenda kulimaliza mapema, tumejipanga vizuri. Ahsante sana.