Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 52 2021-04-12

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na wa kazi wa Mtaa wa Kinyambi na Bugosi katika Halmashauri ya Mji wa Tarime?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali na kwa ruhusa yako naomba nimshukuru Mungu kwa afya na kuniwezesha kusimama hapa. Kwa vile ni mara yangu ya kwanza kipekee nimshukuru sana Mheshimiwa Rais mama yetu mama Samia Suluhu Hassan kwa kuniacha niendelee kutumika kwenye Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kama Waziri. Baada ya shukrani hizo naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Kambaki Michael Mbunge wa Tarime Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wananchi waliokuwepo kabla ya eneo kuchukuliwa na Jeshi hawajalipwa fidia. Uthamini uliofanywa na Halmashauri ya Tarime ulikamilika na ambapo kiasi cha shilingi 1,651,984,692.76 zilihitajika. Jedwali lilipelekwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali mwezi Machi 2020 kupata idhini na lilirejeshwa Tarime kwa marekebisho.

Mheshimiwa Spika, mwezi Machi, 2021 Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa iliwasiliana na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na majibu yaliyotoka ni kwamba, uthamini huo utarejewa kwa kuwa ulifanywa kwa muda mrefu na pia baadhi ya nyaraka zilikosekana kuhalalisha fidia hiyo.

Mheshimiwa Spika, Wananchi wa Mtaa wa Kinyambi na Bugosi wanaombwa wawe na Subira katika kipindi hiki ambacho Halmashauri inafanya taratibu za kurejea uthamini huo. Utaratibu wa uthamini utakapokamilika Serikali italipa fidia kwa wananchi hao kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi.