Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Barabara za kutoka Kata ya Kalenga kuelekea kata za Ulanda, Maboga, Wasa, Kihanga hadi Kijiji cha Mwambao ni mbovu sana: - Je, ni lini Serikali itahakikisha barabara hizi zinapitika hata kwa kiwango cha changarawe?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Kata hizo ambazo nimezitaja Kata ya Maboga, Kata ya Kalenga, Kata ya Ulanda, Kata ya Wasa wananchi ni wakulima ambao wanalima mali mbichi nyingi sana; viazi, njengere, maharage na mengine mengi na barabara imekuwa ni kikwazo katika kusafirisha hizo mali zao, na wamekuwa wakipata tabu mali zinaharibikia njiani. Mwaka 2020 pesa alizosema zimetolewa walikwangua sababu ilikuwa ni wakati wa uchaguzi, na sasa hivi baraba hazipitiki.

Je? Kwa nini Serikali haioni kwamba hii barabara sasa imekuwa ni kubwa na inahudumia watu wengi ambayo inaweza ikaenda mpaka ikatokea Madibila Mbeya ili iingie katika mpango wa TANROADS na itoke TARURA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna barabara ambayo wananchi wametumia nguvu zao ambayo imetobelewa kutoka katika Kata ya Kihanga ikaja katika Kata ya Maboga ambako kuna Zahanati na kuna Hospitali ya Wilaya iliyoko Tosamaganga, wananchi wanashindwa kufika kupata hudama hizo.

Je, ni lini sasa Serikali itaifanyia kazi barabara hii ili wananchi hawa waweze kupata huduma hizo za afya na kuweza kufika katika maeneo hayo kwa urahisi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ameuliza kwamba kwa nini Serikali sasa isione umuhimu wa kuihamisha barabara ambayo inapita Maboga, Kalenga, Wasa, Kihanga mpaka kutokea Madibila kutoka TARURA kwenda TANROADS.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie kabisa kwamba si barabara zote zinahitaji kupandishwa kwenda na kuhudumiwa na TANROAD, lakini jambo kubwa ambalo naweza nikamuhakikishia ni kwamba kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, Serikali itaendelea kuzitengea fedha barabara zote za muhimu.

Mheshimiwa Spika, na kikubwa ambacho alikuwa amekisema Serikali haifanyi kazi wakati wa uchaguzi peke yake, Serikali inafanya kazi muda wote, na katika bajeti hizi tumetenga fedha kwa ajili ya kazi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la pili ameuliza vilevile barabara ya kutoka Kihanga kwenda Maboga ambako amesema kuna kituo cha afya ni lini Serikali itahakikisha kwamba barabara hiyo inajengwa, nimeeleza hapa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na kwa sababu fedha tumetenga katika bajeti na kwa sababu bajeti tunakwenda kupitisha sisi sote hapa nikuombe Mheshimiwa Mbunge tupitishe hiyo bajeti ili barabara zetu zitengenezwe, ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Barabara za kutoka Kata ya Kalenga kuelekea kata za Ulanda, Maboga, Wasa, Kihanga hadi Kijiji cha Mwambao ni mbovu sana: - Je, ni lini Serikali itahakikisha barabara hizi zinapitika hata kwa kiwango cha changarawe?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza lakini pia namshukuru dada Grace kwa kuuliza swali ambalo tulikuwa tunajadiliana juu ya barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, aa ninacho…

SPIKA: Mheshimiwa Jackson kwa hiyo swali hili ulimtuma kumbe ee!

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, tunajadiliana, mimi na yeye tunafanya kazi kwa kushirikiana na kwa tunajadiliana; lakini amewahi kuuliza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la nyongeza ni kuhusu barabara inayotoka Kijiji cha Wenda kwenda Lupembelwasenga inatokea Mgama. Barabara hii kwa taarifa nilizonazo ilikuwa imetengewa fedha katika ule mpango wa European Union, na tayari nilishauliza RCC lakini sikupata majibu yanayoridhisha.

Je, Serikali inaweza kunipa majibu sasa, kwa kuwa barabara hii ni muhimu kwa sababu ya wakulima wanaotoka maeneo hayo na kuyawaisha kufika kwenye barabara hizi za lami ili awahi huku Dodoma? Ni lini sasa Serikali inaweza kututengenezea? Ahsante sana.

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, barabara hiyo tumeichukua na tutaifanyia upembuzi ili tuone kama inakidhi vigezo vya kuhama ili tuihamishe iende TANROADS naomba kuwasilisha.