Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 51 2021-04-12

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:-

Barabara za kutoka Kata ya Kalenga kuelekea kata za Ulanda, Maboga, Wasa, Kihanga hadi Kijiji cha Mwambao ni mbovu sana: -

Je, ni lini Serikali itahakikisha barabara hizi zinapitika hata kwa kiwango cha changarawe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2019/ 2020 Serikali kupitia TARURA katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ilichonga tuta la barabara lenye kilometa 25 iliyozinufaisha Kata za Maboga, Wasa na Kalenga kwa gharama ya Shilingi milioni153. Vile vile TARURA ilifanya matengenezo ya kawaida kwenye barabara ya Magubike, Igangindung’u yenye urefu wa kilomita nane iliyovinufaisha Vijiji vya Kihanga na Mwambao kwa gharama ya Shilingi milioni 69.17. Katika mwaka wa fedha 2021 barabara hizo zimetengewa kiasi cha Shilingi milioni 54 kwa ajili ya matengenezo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kujenga na kukarabati miundombinu ya barabara na madaraja nchi nzima kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.