Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Katika hali halisi hiyo pesa iliyotengwa 1.5 kwa ujenzi wa barabara ya lami ni ndogo sana na upembuzi yakinifu umefanyika muda mrefu sana.

Je, Serikali haioni haja ya kuongeza pesa angalau hata kidogo, watutengenezee hata kilometa 30 tu, kwa mwaka huu, halafu na zile zitakazobakia waongoze pesa kwa mwaka ujao watutengenezee? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hela iliyotengwa ni hela ndogo kulingana na urefu wa barabara, lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii fedha iliyotengewa ni fedha ya awali kwa ajili ya mobilization na kadri fedha itakavyoendelea kupatikana kwa jinsi Serikali itakavyopata, itazidi kuongezewa ili kujengwa kwa kiwango chote.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii inatakiwa ijengwe katika kipindi cha awamu yote hii ya miaka mitano. Kwa hiyo, kadri fedha itakavyoendelea kupatikana basi barabara hii tunahakika kwamba itajengwa yote kwa kiwango cha lami, kwa maana ya Masasi, Nachingwea hadi Liwale. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii barabara siyo kwamba fedha Serikali hawana ya kujenga, ninachokiona hapa ni kwamba Serikali bado haijaamua kujenga hii barabara, kwa sababu zipo barabara zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2018, mwaka 2017, mwaka 2016 zimeshajengwa na zingine zinajengwa. Lakini hii tangu mwaka 2014, ninaiomba Serikali iamue kwa maksudi kabisa kuikomboa Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Nachingwea ili iweze kufunguka nasi kiuchumi tuweze kuwa miongoni mwa watu waliopo duniani.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya vitu ambavyo vinaongoza katika kutengeneza hizi barabara kwa kweli ni uwezo wa Serikali kwa maana ya bajeti, lakini Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ahadi za viongozi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nachingwea - Liwale kwenye Ilani yetu ni kati ya barabara ambazo zipo kwenye usawa wa kilometa 7,500 ambazo zinatakiwa zikamilishwe usanifu wa kina kazi ambayo tayari imefanyika. Kwa hiyo ni hatua ya awali ambayo imefanyika na sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, usanifu tayari umekamilika kama ilivyoahidiwa kwenye bajeti mwezi Juni mwaka huu. Kwa hiyo, tayari Serikali imeshapiga hatua na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Liwale kwamba kwa kuwa tayari tumeshaanza kadri fedha zitakapopatikana naamini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Kuchauka ameonesha masikitiko yake makubwa kabisa, naamini nasi umetupa nafasi kwa maana ya Wabunge wa Nachingwea, Ndanda, Masasi na maeneo mengine kwenye umuhimu wa hii barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nami nimuulize Mheshimiwa Waziri, Wizara imetenga shilingi bilioni 1.5 tu, kwa makisio ya sasa ni kama kilometa moja na nusu, wanapotaka kuanza kujenga barabara hii wataanzia kujenga upande gani? kwa sababu shida ipo Masasi, shida ipo pia Nachingwea. Watueleze wanataka kuanza kujenga upande gani kwa pesa kidogo namna hiyo waliyoitenga. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwambe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara tunachojenga ni kilometa hizo 45 kati ya Masasi na Nachingwea. Lakini hata ukianza Masasi, ukianza Nachingwea bado barabara ni ileile mtu atakapopita, atapita kokote. Nadhani nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la kuanza wapi ama wapi nadhani isingekuwa ni hoja kubwa cha msingi tukamilishe hizo kilometa 45 kwa sababu hata kama itaanzia Masasi, itaanzia Nachingwea, lakini atakayepita, atapita tu kwenye hiyo barabara.

Mheshimiwa Spika, nadhani hilo aiachie Wizara na wataalam wataangalia pia wapi tunapofanya mobilization inaweza kuwa ni rahisi, jambo la msingi tukamilishe hizo kilometa 45. Ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyopo kule Liwale, Nachingwea yanafanana kabisa na yaliyopo katika Jimbo la Manyoni Magharibi Mkoa wa Singida kuunganishwa na Mkoa wa Mbeya kwa barabara inayotoka Mkiwa, Itigi hadi Rungwa.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Massare Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba katika bajeti tuliyopitisha barabara hii ya kuanzia Mkiwa kwenda Rungwa, Lupa hadi Makongorosi, imetengewa bajeti kuanza kwa kiwango cha lami. Na sisi kama Wizara tunategemea muda wowote barabara hii iweze kutangazwa kwa ajili ya ujenzi, kwa sababu ni kati ya barabara chache ambazo zimebaki ambazo ni barabara kuu, trunk, yaani kuunganisha Mkoa wa Singida na Mkoa wa Mbeya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba taratibu zote za manunuzi zimeshakamilika, tunachosubiri ni kutangaza hiyo tender kwa sababu fedha imeshapitishwa na Bunge lililopita kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.