Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 60 2021-09-06

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY K. MSONGWE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Masasi hadi Liwale kupitia Nachingwea kwa kiwango cha lami ambapo kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa sehemu ya Masasi – Nachingwea – Nanganga yenye urefu wa kilometa 90 ilikamilika mwaka 2014 na sehemu ya Liwale – Nachingwea yenye urefu wa kilometa 130 imekamilika mwezi Juni, 2021. Katika mwaka huu wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 1,500 yaani sawa na shilingi bilioni 1.5 zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya Masasi – Nachingwea.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili kuhakikisha inaendelea kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka huu wa fedha wa 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 634 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali.