Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA Aliuliza:- (a) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa wanafunzi wote kunufaika kwa 100% bila kujali shule walizosoma? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wazazi waliostaafu ambao wameshindwa kuchangia gharama za elimu ya juu?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana ningependa nimuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwanza ningependa kujua katika bajeti yao ya mwaka huu wa 2021 ni wanufaika wangapi ambao wataweza kunufaika na mikopo hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili nilikuwa napenda niulize Serikali ina mpango gani wa kuwezesha wanafunzi ambao wako vyuo vya kati ambao wale ndio wenye mahitaji makubwa zaidi ya hii mikopo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Naibu Spika, ahsante na napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyoeleza katika bajeti yetu wakati tunapitisha katika Bunge la Bajeti kwamba bajeti ya Bodi ya Mikopo imeweza kupanda kutoka shilingi bilioni 464 mwaka 2021 mpaka shilingi bilioni 570 mwaka 2122 na kwa hali hiyo basi wanufaika wa bodi watapanda kutoka 149,000 wale ambao walinufaika katika kipindi kilichopita mpaka kufika 160,000 katika mwaka 2021/2022 katika mchanganuo kwamba wale wanaoendelea 98,000 watakuwa wanaoendelea 62,000 tunakadiria katika watakaodahiliwa katika mwaka wa kwanza. Kwa hiyo kwa ujumla wao watakaonufaika tunakadiria kuwa watakuwa sio chini ya 160,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili amezungumzia kuhusiana na suala la wanafunzi wa vyuo vya kati. Kutokana na ufinyu wa bajeti yetu bado hatujaweza kuwafikia wanafunzi hawa wa vyuo vya kati kwa hiyo naomba tulichukue kama Serikali jambo hili wakati tunaboresha bajeti yetu kama Serikali, lakini ninyi Wabunge ndio ambao tunapitisha bajeti hapa, basi tunaweza kulileta mezani kwa ajili ya mjadala ili tuweze kuona namna gani tunaweza kuwafikia wale wa kada ya kati. Lakini kwa mujibu wa sheria sasa hivi bodi hii inashughulikia wale wa elimu ya juu peke yake, ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA Aliuliza:- (a) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa wanafunzi wote kunufaika kwa 100% bila kujali shule walizosoma? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wazazi waliostaafu ambao wameshindwa kuchangia gharama za elimu ya juu?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Pamoja na kazi nzuri iliyofanywa na Serikali ya kugharamia elimu kutoka chekechea mpaka kidato cha nne na utaratibu unaofanywa na Serikali wa kutoa mikopo kwa elimu ya juu bado hapa vijana wa kidato cha tano na sita kuna tatizo la kugharamia elimu.

Ni lini Serikali itaweka sasa utaratibu ili kuwahusisha vijana wa kidato cha tano na sita katika utaratibu wa elimu bila malipo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Naibu Spika, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nape kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli vijana wetu wa kidato cha tano na sita wanatakiwa kugharamia kwa maana ya ada kwa wale wa kidato cha tao na sita ambao kwa wanafunzi wetu wa bodi kulipa shilingi 70,000 na wale wa
day kulipa shilingi 35,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii tunaiona kwamba ni affordable au inaweza sana Watanzania wengi kuilipa lakini kwa vile Mheshimiwa Mbunge ameielezea hapa acha basi tulibebe jambo hili tuweze kwenda kuliangalia kwa kina kama Serikali, kwa vile Serikali sasa imeanza kutoa elimu bila malipo kutoka elimu ya awali mpaka kidato cha nne basi na hili tuliingize kwenye mjadala tuweze kuliangalia katika kipindi kijacho kama tunaweza kama Serikali tukaweza ku-wave na kuweza kuondoa ada hii kwa upande wa kidato cha tano na sita, aHsante.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA Aliuliza:- (a) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa wanafunzi wote kunufaika kwa 100% bila kujali shule walizosoma? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wazazi waliostaafu ambao wameshindwa kuchangia gharama za elimu ya juu?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY A. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; Serikali kama kawaida imekuwa ikifanya kazi kubwa sana kwenye elimu. Sasa hivi imetokea wanafunzi wanaotoka kidato cha nne wanachaguliwa moja kwa moja kwenda kwenye vyuo.

Sasa nilitaka kuuliza na wengine hawana uwezo kabisa na wazazi wao wameshindwa kuwalipia na utakuta ana division one au two. Sasa nilitaka kuuliza je, Serikali inawasaidiaje hawa vijana ambao wanashindwa uwezo wa kwenda huko vyuoni kwa ajili ya kuwasaidia wafike huko vyuoni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Naibu Spika, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jumbe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Jumbe anazungumza kwamba wapo wanafunzi ambao wanafaulu lakini nafasi za kujiunga kwenye elimu ya juu zimekuwa ni changamoto na suala kubwa hapa ni kuweza kufanya upanuzi. Nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Jumbe na Wabunge wote kwamba tumesaini sasa mkopo kutoka Benki ya Dunia katika mradi wetu wa HIT ambao zaidi ya dola za Kimarekani milioni 425,000 ambazo zinakwenda kufanya upanuzi mkubwa pamoja na ukarabati wa miundombinu katika vyuo vikuu. Tutakapofanya ukarabati huu tunaamini tutaongeza nafasi za udahili na kuondoa changamoto hii ya wanafunzi wengi ambao wamefaulu vizuri lakini kuachwa kwenye vyuo vyetu. Nafasi hizo zitakapoongezeka tunaamini wanafunzi hawa wote ambao watakaofaulu wataweza kupata nafasi ya kwenda kuingia katika vyuo vyetu, asante sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA Aliuliza:- (a) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa wanafunzi wote kunufaika kwa 100% bila kujali shule walizosoma? (b) Je, Serikali inawasaidiaje wazazi waliostaafu ambao wameshindwa kuchangia gharama za elimu ya juu?

Supplementary Question 4

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini niseme ukweli kwamba mikopo inayotolewa ni mikopo na si zawadi. Sasa kuna kitu ambacho kimejitokeza kwamba watu wanaosoma shule binafsi au watoto wa watumishi wa Serikali hawapati mikopo huo ndio ukweli tusiseme uongo.

Je, wako tayari kama itajirudia tena hiyo kitu walete sheria Bungeni ibadilishwe ili itamke wazi kwamba watakaopewa mikopo ni watu waliosoma Serikalini na sio waliosoma kwenye shule za watu binafsi au watoto wa watumishi wa Serikali? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Naibu Spika, ahsante na napenda kujibu swali dogo la Mheshimiwa Ndakidemi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi mikopo hii inaratibiwa kwa ile Sheria Namba 178 ya Bodi ya Mikopo ambayo imebainisha vigezo na vielelezo vya mwanafunzi gani na mwenye sifa zipi wa kupata mikopo hiyo na ambayo haibainishi kwamba amesoma shule gani na alikuwa analipa ada gani katika hizo shule za nyuma zilizopita. Lakini kwa vile yeye Mheshimiwa Mbunge amelieleza jambo hili hapa, tunalichukua tunakwenda kulifanyia kazi na kama kulikuwa na mchezo fulani ambao unachezwa nimwahidi tu kwamba katika kipindi hautatokea na mikopo hii itawafikia wote wenye uhitaji wa kupata mikopo hii.