Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 45 2021-09-03

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA Aliuliza:-

(a) Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa wanafunzi wote kunufaika kwa 100% bila kujali shule walizosoma?

(b) Je, Serikali inawasaidiaje wazazi waliostaafu ambao wameshindwa kuchangia gharama za elimu ya juu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu: -

Mheshimwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Jimbo la Chumbuni lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo (SURA 178) ambayo inaelekeza kuwa walengwa wa mikopo hiyo ni wahitaji (needy).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa uhitaji wa mwanafunzi hupimwa kwa kuchambua taarifa zilizowasilishwa wakati wa maombi ya mkopo, zikiwemo gharama za masomo ya sekondari au stashahada. Uchambuzi huu hutumia king’amua uwezo (means testing tool) ambacho hubaini kiwango cha uhitaji cha mwombaji mmoja mmoja ukilinganisha na wengine.

Aidha, uhitaji wa mnufaika unatumika kuamua kiasi anachopangiwa kulingana na gharama ya shahada aliyodahiliwa. Baada ya uchambuzi linganishi, waombaji hupangiwa mikopo kulingana na uhitaji wao. Katika mwongozo, vigezo na sifa za kunufaika na mikopo ya elimu ya juu, hakuna kigezo mahususi cha shule aliyosoma mwombaji na mnufaika.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu waombaji wa mikopo ambao wazazi wao wamestaafu katika utumishi, Serikali inaamini utaratibu wa sasa wa kutambua na kuwapangia mikopo wahitaji wanaotoka katika familia zisizo na uwezo wa kumudu gharama za elimu ya juu kwa watoto wao unajitosheleza. Hata hivyo, Serikali ipo tayari kuendelea kupokea maoni ya namna ya kuboresha zaidi utaratibu huu.