Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa muda mrefu wa kuwatambua na kulinda maslahi ya vijana waliojiajiri katika sanaa ya burudani kama Video Vixen na Video King?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nitumie nafasi hii kushukuru majibu mazuri sana ya Serikali. Swali langu la nyongeza;

Je, Serikali ina mpango gani wa kutambua kundi la Video Vixens kama makundi mengine ya sanaa kupitia Sheria Na. 7 ya Mwaka 1999; kwa sababu Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba tayari kundi hili halitambuliki rasmi bali kundi linalotambulika ni kundi la wanamuziki; na kwamba mikataba ya watu hawa haitambuliki, kwamba inayotambulika ni ya kundi la wanamuziki pamoja na makundi mengine, na siyo kundi la Video Vixens? Je, kupitia Sheria hiyo Na. 7 ya Mwaka 1999 tunawasaidiaje vijana hawa kuweza kutambulika?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa kundi la Video Vixens ambalo linachukua Video Kings pamoja na Queens, na kwamba ni kundi linalochukua vijana wengi zaidi; sasa Serikali haioni haja ya kuwasaidia kuwatengenezea mikataba mizuri ili vijana hawa wasipitie changamoto wanazozipitia; kwa sasa hivi kwa sababu wanafanya kazi kubwa lakini wanalipwa ujira mdogo na wananyanyasika?

Nikisema wananyanyasika nadhani Waheshimiwa Wabunge tunaelewana. Ahsante sana.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asia kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwenye majibu yangu ya awali na ya msingi nilieleza kwamba kwenye Sheria yetu ya Mwaka 1999 vijana hawa walikuwa hawajatambuliwa, lakini kwa sababu ya umuhimu wa kazi yao; ilibidi sheria hii tuirekebishe mwaka 2019, Kifungu na. 47(b) ndicho kikatambua sasa ikaingiza mkataba, kwamba ni lazima hawa vijana ambao wana-perform na wale owners wa kazi ile waweze kutambuliwa, na mikataba yao COSOTA iiangalie.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilihakikishie Bunge lako Tukufu na wasanii kwamba hawa vijana hawajaachwa, sheria inawatambua. Na hata pale ambapo vijana hawa wanadhulumiwa COSOTA inaingilia kati kwa sababu ile mikataba inakuwa imeshapitia kwao. Mimi niwahakikishie kwamba wakati tunafanya marejeo ya kanuni maoni yamechukuliwa kote na hatujapata malalamiko so far kwamba wanaonewa.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuendelea kuwalinda kwa sababu – swali lake la pili – tunapitia Kanuni yetu ya mwaka 2003 kuona jinsi gani tuboreshe mpaka hata mgawanyo tunaotoa wa fedha kwa wamiliki au wasanii wetu; maana kama kuna jambo lolote within marekebisho yale Mheshimiwa Mbunge, yatakwenda kuangaliwa wakati Kanuni hiyo haijafika mwisho, maana wana nafasi ya kutoa tena maoni yao.