Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo Kikuu katika Mkoa wa Kagera?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninayo maswali mawili.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kagera ni mkoa mkubwa, una watu zaidi ya 3,000,000 lakini hadi leo hauna Chuo kikuu hata kimoja. Vipo vyuo vikuu vilikuwa vimeanzishwa na Mashirika ya Dini, moja ni Lutheran, walianzisha kile cha Joshua Kibira; Roman Catholic walianzisha branch ya Saint Augustine lakini vyote Serikali ilivifunga: Kwa kuwa Serikali inasema kuanzisha Vyuo Vikuu ni gharama, badala ya Serikali kuvifunga, haioni ingekuwa ni vizuri wakaendelea kuvijenga, kuvipa miongozo na kuviwezesha hivi vilivyoanzishwa badala ya kuvifunga? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; miaka ya nyuma huko Mkoa wa Kagera ulikuwa unawika kwenye elimu, uko katika the best three, lakini sasa hivi haiko hivyo: Je, Serikali haioni kwamba sasa wakati umefika, angalau waanzishe tawi moja la Chuo Kikuu cha Serikali kama Sokoine, kama Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mkoa wa Kagera ili kuchochea maendeleo ya Mkoa huo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benardetha Mushashu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Kagera tulikuwa na vyuo vikuu binafsi viwil,i hivyo alivyovizungumza Mheshimiwa Mushashu; hicho cha Kadinali Rugambwa na kile cha Kibira alichokizungumza. Nikuthibitishie mbele ya Bunge lako Tukufu, Chuo hiki cha Kadinali Rugambwa hakikufungwa, badala yake walihamisha usajili kutoka ule wa TCU kwenda ule wa NACTE. Kwa hiyo, chuo hiki kipo, kinaendelea kutoa huduma pale, ingawa hazitoi zile kozi za degree, badala yake zinatoa zile kozi za kawaida, za chini, lakini bado kinaendelea kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, kwenye hiki chuo cha pili cha Kibira, wenyewe wamiliki wa chuo hiki waliomba kifungwe kutokana na kushindwa wao wenyewe kuendesha chuo hiki. Kwa hiyo, nimshawishi tu Mheshimiwa Mbunge aweze kuwasiliana na wamiliki wa chuo hiki waweze kujipanga vizuri ili sasa waje kufanya maombi upya kama upo uhitaji wa kukifungua chuo hiki kama wataona inafaa, nasi tuko tayari kupokea maombi yao.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la pili la vyuo vyetu hivi vikuu kuanzisha matawi kwenye eno hilo, ni suala ambalo linakubalika, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, lakini inatakiwa sasa ifanyike ile needs assessment kwa vyuo hivi vyenyewe kwa sababu wana mamlaka ya kufanya hivyo kama wanaona uhitaji huo wa kuanzisha branch hizo uko katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutawafikishia ujumbe huu waweze kuja Kagera wafanye market analysis pamoja na needs assessment ili kuona kweli kama upo uhitaji wa kuanzisha branch kwenye maeneo hayo, waweze kufanya hivyo. Ahsante. (Makofi)