Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 27 2021-09-01

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo Kikuu katika Mkoa wa Kagera?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Benardetha Kasabago Mushashu Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kutokana na gharama kubwa za uwekezaji unaohitajika katika kuanzisha Vyuo Vikuu, ni vigumu kwa Serikali kuanzisha Chuo Kikuu katika kila Mkoa. Vyuo Vikuu vya Serikali na Binafsi vilivyopo nchini vinapokea wanafunzi kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na vilevile kutoka nje ya nchi ambapo ndiyo utamaduni wa Vyuo Vikuu Duniani.

Mheshimiwa Spika, katika Mkoa wa Kagera kuna tawi la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilichopo katika Makao Makuu ya Mkoa ambacho ni cha Serikali. Kwa sasa Serikali inaendelea na mpango wa kuboresha Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu zilizopo kwa kukarabati na kujenga miundombinu mipya pamoja na kuongeza vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia ili kuongeza nafasi ya udahili na kuongeza ubora wa elimu ya juu itolewayo ili kukidhi mahitaji ya nchi. Ahsante.