Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha Polisi Bububu ambacho ni chakavu sana?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja tu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuendeleza kituo hiki kwa sababu kituo hiki ni chakavu, cha siku nyingi na kibovu. Sasa naiomba Serikali tufuatane, tuongozane na Waziri ili akajionee mwenyewe katika kituo hicho cha Bububu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze kwa juhudi kubwa anayoifanya na najua anataka kile kituo kifanyiwe ukarabati ili kiweze kutoa huduma kwa sababu jimbo lake ni jimbo ambalo lina harakati nyingi za kiutalii ambazo zinachangia pato kubwa la Taifa. Kwa hiyo harakati hizi sometime zinakuwa zinapelekea athari za kiusalama.

Mheshimiwa Spika, kikubwa nimwambie tu Mheshimiwa kwamba nipo tayari kufuatana naye kwenda kukagua kituo kile chumba kwa chumba, eneo kwa eneo ili kuona wapi panahitaji marekebisho na tuko tayari kama Serikali kukirekebisha kituo kile. Nakushukuru.