Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 24 2021-09-01

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha Polisi Bububu ambacho ni chakavu sana?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Jimbo la Bububu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uchakavu wa Kituo cha Polisi Bububu na tayari tathmini kwa ajili ya ukarabati imefanyika mwezi Mei, 2021 na fedha kiasi cha shilingi 33,172,200 zinahitajika kwa ajili ya kubadilisha paa, mfumo wa umeme, mfumo wa maji taka na maji safi, pamoja na kupaka rangi. Aidha, Serikali inatafuta fedha za ukarabati wa kituo hicho ikiwa ni pamoja na vituo na makazi ya askari ya maeneo mengine ambayo yanafanyiwa tathmini kwa ajili ya ukarabati. Ahsante.