Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa muhimu kwenye hospitali inayojengwa katika Mji wa Tunduma ili ianze kufanya kazi mapema? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza madaktari na wakunga pamoja na kuongeza bajeti katika Kituo cha Afya cha Tunduma ili kukidhi mahitaji ya kituo?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri ambayo imeweza kunijibu, lakini kiupekee kabisa nataka nitoe angalizo kwa Serikali kwamba Kituo cha Afya Tunduma asikichukulie kama vituo vingine ambavyo viko nje ya mpaka wa Tunduma kwa maana mahitaji yake yanakuwa ni makubwa zaidi, kwa hiyo anaposema kwamba ataweza kupunguza watumishi Tunduma tena awapeleke kwenye hospitali hiyo inayojengwa naona kama bado changamoto itakuwa kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ninapenda niulize maswali yangu mawili ya nyongeza; ni lini hasa Serikali itaweza kuanzisha huduma katika hii hospitali inayojengwa ambayo ameweza kutuonesha kwamba asilimia 82 ya ujenzi imeshafanikishwa. Kwa hiyo, ninatamani kujua ni lini hasa huduma zitaanza kutolewa pale?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ninapenda kufahamu mahitaji ya kituo cha afya kulinga na na nature ya watu wa pale tunahitaji madaktari, na madaktari aliyosema nina uhakika ni hao madaktari wawili ambao wanasubiria Hospitali ya Wilaya ianze kufaya kazi.

Sasa basi ninatamani kujua ni lini hasa Serikali itpeleka madaktari na wauguzi wakunga, siyo wahudumu wa afya kama walivyoweza kuanisha kwenye majibu yao, mahitaji yetu ni madaktari na wauguzi wakunga, specifically hapo ninapenda kupata majibu. Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kumhakikishia Mheshimiwa Mwandabila kwamba Serikali inakichukulia kwa umuhimu wa hali ya juu sana Kituo cha Afya cha Tunduma kwa sababu ya idadi ya wananchi wanaohudumiwa katika kituo kile na ndiyo maana katika maelezo yangu ya msingi nimeeleza namna ambavyo Serikali imepeleka watumishi wengi sana, watumishi 22 wa ziada ukilinganisha na ikama ya mahitaji ya kituo cha afya, na hiyo ni dalili kwamba Serikali inajali na kuthamini sana huduma za Kituo cha Afya cha Tunduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba kwa sababu tunaendelea na ujenzi wa Hospitali ya Mji wa Tunduma, kwa vyovyote vile, idadi ya wagonjwa watakaotibiwa katika kituo cha afya itapungua na wengine watakwenda kutubiwa katika Hospitali ya Mji wa Tunduma itakapokamilika. Kwa hiyo, ile idadi ya wagonjwa ambayo itaondoka Kituo cha Afya cha Tunduma itakwenda kuhudumiwa katika hospitali ya mji na watumishi hawa waliopo. Lakini pia Serikali itakwenda kuajiri watumishi wengine kama ambavyo mpangio upo katika mwaka wa fedha ujao ili tuweze kuongeza watumishi katika hospitali ile ya mji lakini pia katika Kituo cha Afya cha Tundma.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Hospitali hii ya Mji wa Tunduma inayojengwa inatarajia kuanza huduma za awali za OPD ifikapo tarehe 27 Aprili, 2021 ili wananchi wetu waanze kupata huduma za awali za OPD wakati shughuli za umaliziaji na ujenzi wa miundombinu mingine inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa muhimu kwenye hospitali inayojengwa katika Mji wa Tunduma ili ianze kufanya kazi mapema? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza madaktari na wakunga pamoja na kuongeza bajeti katika Kituo cha Afya cha Tunduma ili kukidhi mahitaji ya kituo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa Kituo cha Afya cha Nakatunguru pale Ukerewe kilishakamilika kujengwa na kukamilika kwake kutasaidia sana kupunguza mzigo kwenye Hospitali yetu ya Wilaya; ni lini sasa Serikali itapeleka wataalam na vifaa tiba ili Kituo hiki cha Afya cha Nakatunguru kianze kufanya kazi na kusaidia kutoa huduma kwa wananchi wa Ukerewe?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba katika Jimbo la Ukerewe, Wilaya ya Ukerewe, tayari kituo cha afya kimeshajengwa na kimekwishakamilika na hatua iliyobaki sasa ni kupeleka watumishi na vifaa tiba ili huduma za afya zianze kutolewa katika kituo kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe kwamba Serikali inatambua na tumeshaweka mipango kwanza kuhakikisha katika Halmashauri ya Ukerewe tunapata watumishi wachache kwa maana ya internal redistribution ya watumishi waliopo na vifaa tiba kwa uchache vilivyopo kwa ajili ya kuanza huduma.

Lakini pili, mpango uliopo katika mwaka wa fedha ujao ni kutenga fedha kwa ajili ya kununua vifaa tiba, lakini pia kadri tutakavyoajiri watumishi, tutawapangia katika Halmshauri ya Ukerewe na katika kituo kile cha afya ili kiweze kutoa huduma bora kwa wananchi. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo tumelichukua, tunalifahamu na tunalifanyia kazi.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa muhimu kwenye hospitali inayojengwa katika Mji wa Tunduma ili ianze kufanya kazi mapema? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza madaktari na wakunga pamoja na kuongeza bajeti katika Kituo cha Afya cha Tunduma ili kukidhi mahitaji ya kituo?

Supplementary Question 3

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.

Kwa kuwa katika Jimbo la Vwawa kuna Kituo cha Afya ambacho kimejengwa kwenye Tarafa ya Iyula ambacho kimekamilika karibu miaka miwili iliyopita, lakini mpaka sasa hivi hakina watumishi wa kutosha na hakina vifaa.

Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba watumishi wa kutosha wanapelekwa na vifaa vya kuweza kuwasaidia kutoa huduma mbalimbali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba sote tunafahamu kazi kubwa sana iliyofanywa na Serikali yetu katika kuboresha miundombinu ya huduma za afya kwa kujenga vituo vya afya takribani 487 ndani ya miaka mitano iliyopita, lakini harakati hizo za ujenzi zinaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba katika maeneo mbalimbali bado tuna changamoto ya idadi ya watumishi wanaohitajika kuanza kutoa huduma, lakini pia tuna changamoto ya vifaa tiba, na ndiyo maana katika mpango wetu wa vituo vya afya katika mwaka wa fedha ujao tunatarajia kuomba takribani shilingi bilioni 22.5 kwa ajili kwanza ya kuhakikisha vituo vyote na hospitali za halmashauri zilizojengwa zinapata vifaa tiba kwa kushirikiana na mapato ya ndani ya halmashauri. Lakini pili, mpango upo wa kwenda kuwaajiri watumishi kwa ajili ya kuwapeleka katika vituo hivyo.

Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Hasunga na Waheshimiwa Wabunge wote wenye hoja kama hiyo, kwamba Serikali ina takwimu za kutosha za mahitaji ya vifaa tiba katika vituo vyetu vya afya, za mahitaji ya watumishi katika vituo hivyo vya afya na itakwenda kuajiri watumishi kwa kadri ya upatikanaji wa fedha lakini pia tutakwenda kupeleka vifaa tiba. Kwa hiyo, Mheshimiwa Hasunga nikuhakikishe kwamba kituo hicho cha afya kipo kwenye mpango na tutahakikisha kinaanza kutoa huduma bora kwa wananchi.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa muhimu kwenye hospitali inayojengwa katika Mji wa Tunduma ili ianze kufanya kazi mapema? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza madaktari na wakunga pamoja na kuongeza bajeti katika Kituo cha Afya cha Tunduma ili kukidhi mahitaji ya kituo?

Supplementary Question 4

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nakushukuru. Napenda kuiuliza Serikali kuhusiana na Kituo cha Afya pale Kigogo ambacho kinahudumia Wilaya tatu za Ubungo, Ilala na Kinondoni yenyewe, lakini tuna shida kubwa ya jokofu la kuhifadhia maiti. Tayari Serikali imeshatupatia jokofu lile, lakini limekaa bila ya kuwekwa katika sehemu husika.

Ni lini Serikali itatujengea eneo ambalo tutahifadhia jogofu lile kwa madhumuni ya kuweza kuwahifadhi wenzetu ambao wanatangulia mbele za haki? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Kigogo ni kituo muhimu sana na niseme kwa bahati nzuri, mwanzo wa ujenzi mpaka kinakamilika nilikuwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni. Kwa hiyo, nakifahamu vizuri sana kituo kile kwamba ni muhimu na kinahudumia wananchi wengi sana katika Manispaa ya Jiji la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie katika Halmashauri ambazo zina mapato mazuri na juzi tulipokuwa na Kamati ya LAAC katika Manispaa ya Kinondoni, sehemu muhimu ambayo tuliona ni mfano wa kuigwa katika nchi yetu ni uwekezaji mkubwa wa fedha za mapato ya ndani katika miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaamini kwa uwezo wa makusanyo ya ndani ya Manispaa ya Kinondoni, kazi ya ujenzi wa chumba za kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya cha Kigogo ni jambo linalowezekana. Naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni waweke mpango wa haraka ili waweze kujenga chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya cha Kigogo. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa muhimu kwenye hospitali inayojengwa katika Mji wa Tunduma ili ianze kufanya kazi mapema? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza madaktari na wakunga pamoja na kuongeza bajeti katika Kituo cha Afya cha Tunduma ili kukidhi mahitaji ya kituo?

Supplementary Question 5

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa tatizo lililopo katika Hospitali ya Mji wa Tunduma linafanana na Hospitali ya Uhuru iliyoko katika Wilaya ya Chamwino ya ukosefu wa wafanyakazi pamoja na ambulance na hospitali hii iko kwenye eneo ambalo ni la barabarani na linahitaji sana huduma za dharura kwa ajili ya wagonjwa.

Je, Serikali inatoa maelezo gani kuhusiana na upungufu huu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Hospitali ya Uhuru inayojengwa katika eneo la Chamwino ni hospitali muhimu sana katika kuboresha huduma za afya katika eneo la Chamwino na Jiji la Dodoma kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali inatambua kwamba tunahitaji kupata kwanza watumishi wa kutosha katika hospitali ile kwa sababu ni mpya, ndiyo inakamilika na vilevile inatambua kwamba tunahitaji kupata vifaa tiba na gari la wagonjwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tayari limewekwa kwenye mipango ya utekelezaji ya mwaka wa fedha ujao wa 2021/ 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimhakikishie kwamba tutakwenda kuhakikisha watumishi watakaoajiriwa watapelekwa katika Hospitali ile ya Uhuru. Tutakwenda kuhakikisha kwamba tunafanya utaratibu wa kupata gari la wagonjwa na vifaa tiba ili hospitali ile ianze kutoa huduma kwa wananchi. (Makofi)