Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mtwara Pachani – Nallasi – Tunduru itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri kwa kufanikisha kufanya upembuzi yakinifu na kutengeneza zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara ile kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali imesema inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara hiyo na wananchi walio katika maeneo au waathirika wa barabara hiyo bado wanakiu ya kupata fidia yao kwa ajili ya maeneo hayo. Je, ni lini Serikali itaanza kutoa fidia kwa waathirika wa barabara hiyo kutoka Mtwara Pachani, Lingusenguse, Nallasi mpaka Tunduru mjini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali imetenga shilingi bilioni 2.2 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida kwenye barabara hiyo; na kwa kuwa madaraja manne kwenye barabara hiyo yamezolewa na mvua, Mto Sasawala, Lingusenguse, Mbesa pamoja na Lukumbule. Je, Serikali haioni haja ya haraka kupeleka hizo shilingi bilioni 2.2 ili kukamilisha kurekebisha madaraja hayo yaliyoharibika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la fidia litaanza pale ambapo barabara itaanza kujengwa. Awamu ya kwanza ilikuwa ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi umeshakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa nini fedha ya matengenezo iliyotengwa kwa kuwa madaraja yameshazolewa isipelekwe huko. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Tunduru kwamba mpaka leo asubuhi madaraja yote ya kutokea Tunduru daraja la kwanza la Mbesa, Mchoteka sasa yanaweza yakapitika na hivi leo wameanza daraja kubwa la Mto Sasawala na tunaweka ndani ya muda mfupi daraja hili litaanza kupitika ili kuweza kuunganisha Tunduru na eneo la Mtwara Pachani. Ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mtwara Pachani – Nallasi – Tunduru itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo yanayowapata wananchi wa Tunduru yanafanana kabisa na matatizo ambayo yanawapata wananchi wa Kigamboni katika Mkoa wa Dar es Salaam. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kujenga barabara ya Kibada - Kisarawe Two - Mwasonga - Tumbi Msongani ili kuwasaidia wananchi Wilaya ya Kigamboni waweze kupata unafuu wa usafiri?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam kuhusu barabara za Kigamboni. Hiki ni kipindi cha bajeti na kama tulivyoahidi barabara hizi zitajengwa ndani ya miaka mitano, kwa hiyo kwenye bajeti pengine suala la kuanza usanifu wa awali na wa kina litajitokeza. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hizi kama tulivyoahidi zitajengwa. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mtwara Pachani – Nallasi – Tunduru itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya Mgakolongo kwenda Kigalama mpaka Mlongo inayounganisha na nchi ya Uganda, usanifu wake umeshakamilika muda mrefu. Ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye Ilani na nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira tuone bajeti ambayo tunaiandaa hiyo barabara itashughulikiwaje. Kwa sasa siwezi nikasema chochote maana ndiyo tuko kwenye kipindi cha bajeti, kwa hiyo, naomba awe na subira aone kama barabara yake itajengwa lakini tunatambua ni barabara muhimu sana. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE Aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mtwara Pachani – Nallasi – Tunduru itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Changamoto ya barabara iliyoko Tunduru Kusini inafanana kabisa na changamoto iliyoko wilaya ya Ngara ya barabara ya Murugalama - Lulenge - Mizani yenye urefu wa kilomita 85. Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu swali la nyongeza la kwanza, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hii barabara aliyoitaja ambayo inapita eneo la Mgalama - Lulenge nina hakika zitajadiliwa katika kipindi hiki cha bajeti, kwa hiyo, awe na subira.