Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 6 2021-03-30

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE Aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Mtwara Pachani – Nallasi – Tunduru itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani – Lingusenguse – Nallasi Tunduru yenye urefu wa kilometa 300 kwa kiwango cha lami. Kazi hii ilitekelezwa na Mhandisi Mshauri GEG wa Ureno kwa gharama ya shilingi bilioni 2.559 na ilikamilika mwaka jana (2020). Kwa sasa, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati ujenzi wa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara nchini, inaendelea kuihudumia barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka huu wa fedha 2020/2021, Serikali ilitenga kiasi cha shilingi bilioni 2.293 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hiyo.