Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA Aliuliza:- Serikali iliahidi kufikisha Urambo maji ya Ziwa Victoria na kwa sasa yameshafika Tabora:- (a) Je, ni hatua zipi zimechukuliwa katika kutekeleza azma hiyo? (b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimetengwa katika mwaka huu wa fedha na ni lini maji yatafikishwa Urambo?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naipongeza Serikali kwa majibu mazuri lakini pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hotuba yake aliyoitoa tarehe 30 Mjini Tabora ambayo ilituhakikishia kwamba tutapata maji na baadaye pia kuongezewa zaidi na Mheshimiwa Waziri wa Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali haioni kwamba changamoto kubwa ya maji sasa inakaribia kupata ufumbuzi baada ya kuhakikishiwa kwamba mradi utafika huko, Mheshimiwa Waziri anaweza kuja Urambo kwa sasa hivi akaangalia hali halisi na huenda akaongezea hata maeneo yatakayonufaika na mradi huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tumuandalie mkutano wa hadhara arudishie maneno hayahaya ili wananchi wa Urambo waendelee kuishi kwa matumaini na kushukuru Serikali inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa kwa sababu amekuwa ni mfuatiliaji mzuri sana. Kwa kuwa ahadi ya Mheshimiwa Rais lazima tuitekeleze kwa nguvu zetu zote na Urambo inakwenda kunufaika, niseme niko tayari kuja Urambo na mkutano wa hadhara hapa ndiyo mahala pake. Nitahakikisha naelekeza vema jamii ya Urambo na watamuelewa Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa matatizo ya maji yanakwenda kufikia ukingoni.

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA Aliuliza:- Serikali iliahidi kufikisha Urambo maji ya Ziwa Victoria na kwa sasa yameshafika Tabora:- (a) Je, ni hatua zipi zimechukuliwa katika kutekeleza azma hiyo? (b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimetengwa katika mwaka huu wa fedha na ni lini maji yatafikishwa Urambo?

Supplementary Question 2

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Naomba na mimi niulize swali moja tu, ni lini Serikali ya Chama cha Mapinduzi itakwenda kutekeleza miradi ya visima 10 vilivyochimbwa Jimbo la Singida Magharibi katika vijiji vya Minyuge, Mpetu, Kaugeri, Mduguyu pamoja na Vijiji vya Mnang’ana, Munyu na Irisya ukizingatia Jimbo la Singida Magharibi ni miongoni mwa Majimbo ambayo yana changamoto kubwa sana ya maji? Naomba nipate jibu serious kutoka kwenye Serikali serious. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kingu kutoka Singida Magharibi, kama ifuatavyo:-

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Siyo daktari.

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Nimekutunuku au siyo. Wanasema dalili nje huonekana asubuhi, daktari rudi shule ukapate hiyo profession. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nia ya Serikali ni maeneo yote ambayo yalishafanyiwa usanifu tunakuja kuhakikisha kazi zinafanyika ndani ya wakati. Hivyo visima vyote vitachimbwa kadiri ambavyo vipo kwenye bajeti na maji tutahakikisha hayaishii kwenye kisima bali yanatembea kwenye bomba kuu na kuwafikia wananchi kwenye mabomba yao katika makazi lakini vilevile katika vituo vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya yote yanakwenda kutekelezwa kwa kipindi hiki kilichobaki cha mwaka wa fedha na mwaka wa fedha 2021/2022. Isitoshe nitafika kuona eneo husika na kuleta chachu zaidi kwa watendaji wetu, japo tayari tuna watendaji wazuri katika Wizara na wanafanya kazi vizuri sana. (Makofi)