Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 102 2021-02-10

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA Aliuliza:-

Serikali iliahidi kufikisha Urambo maji ya Ziwa Victoria na kwa sasa yameshafika Tabora:-

(a) Je, ni hatua zipi zimechukuliwa katika kutekeleza azma hiyo?

(b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimetengwa katika mwaka huu wa fedha na ni lini maji yatafikishwa Urambo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepata mkopo kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim ya India ambapo jumla ya Dola za Marekani milioni 500 zitatumika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika miji 28 Tanzania Bara na Zanzibar. Kupitia mkopo huo, Mji wa Urambo ni kati ya maeneo yatakayonufaika na mkopo huo. Kwa sasa utekelezaji wa mradi huo upo katika hatua za manunuzi ya wakandarasi wanaotarajiwa kuwepo eneo la miradi ifikapo Mei, 2021 na utekelezaji wake ni muda wa miezi 24.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali imetenga jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 1.89 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Urambo.