Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA Aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini vijiji vyote vya Wilaya ya Kakonko havijapata umeme? (b) Je, ni lini vijiji hivyo vitapata umeme?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kupeleka huduma kwa wananchi. Tatizo lililojitokeza hapa ni baadhi ya vitongoji hasa katika Mji wa Kakonko kurukwa. Mfano, vitongoji vya Itumbiko, Mbizi, Kizinda, Cheraburo zikiwemo taasisi kama shule za makanisa. Kwa nini taasisi na vitongoji hivi vinarukwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, lini sasa haya maeneo ambayo yamerukwa yatapewa huduma hiyo ya umeme? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce Kamamba, Mbunge wa Kakonko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, vitongoji vya Jimbo la Kakonko havijarukwa isipokuwa Serikali inaendelea kupeleka umeme katika vijiji na vitongoji vyetu kwa awamu. Kwa hiyo, kadri ya upatikanaji wa fedha vitongoji vimekuwa vikipatiwa umeme kulingana na mazingira yalivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari umeme umepelekwa katika vijiji 40 vya Jimbo la Kakonko na wakati tunapeleka umeme katika vijiji hivyo baadhi ya vitongoji vilifikiwa katika awamu ya pili ya REA na awamu ya tatu mzunguko wa kwanza. Sasa awamu ya tatu mzunguko wa pili itapeleka umeme katika vijiji lakini na baadhi ya vitongoji pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Kakonko lipo katika awamu ya pili (b) ya mraji jazilizi wa umeme katika vitongoji. Jumla ya vitongoji 49 vitapatiwa umeme katika Jimbo la Kakonko na mradi huu wa jazilizi unaanza kuanzia mwezi Aprili. Kwa hiyo, kadri ya upatikanaji wa fedha, vitongoji vya Jimbo la Kakonko lakini na vitongoji vingine vingi nchini vitaendelea kupelekewa umeme taratibu ikiwa ni pamoja na taasisi za umma. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA Aliuliza:- (a) Je, ni kwa nini vijiji vyote vya Wilaya ya Kakonko havijapata umeme? (b) Je, ni lini vijiji hivyo vitapata umeme?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukrani kwa Serikali kwa kufungua wilaya ya TANESCO pale Chanika na kumshukuru Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwa kufanya ziara kwenye Jimbo la Ukonga, je, Serikali inawaeleza nini wananchi wa Jimbo la Ukonga ambao mpaka sasa miradi yao ya REA haijakamilika kwenye Kata za Chanika, Zingiziwa, Msongola, Majohe na Kivule? Serikali inatoa tarehe gani wananchi wategemee mradi huu kukamilika? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kwamba miradi ya umeme ya REA awamu ya tatu mzunguko wa pili itaanza mwezi huu wa pili na itakamilika kufikia Septemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwa ujumla kwamba miradi yote ya kupeleka umeme vijijini kwa vijiji 2,150 vilivyokuwa vimebakia havijapata umeme, vyote vitapatiwa umeme katika awamu hii ya tatu mzunguko wa pili ya REA. Baada ya hapo hatutarajii kuwa na kijiji chochote ambacho kitakuwa hakina umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwasihi Waheshimiwa Wabunge waendelee kuwa watulivu na wajiandae kupokea mradi mkubwa wa kupeleka umeme vijijini ambao utakuwa unakmilisha vijiji vyote ambavyo vilikuwa havijapata umeme.