Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 95 2021-02-10

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA Aliuliza:-

(a) Je, ni kwa nini vijiji vyote vya Wilaya ya Kakonko havijapata umeme?

(b) Je, ni lini vijiji hivyo vitapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Buyungu lina jumla ya vijiji 44, vijiji 40 tayari vinapatiwa umeme kupitia awamu ya pili na ya tatu ya utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini. Kazi inayoendelea sasa ni kuunganisha umeme katika vijiji 22 kwa wateja ambavyo vilipata umeme tayari ili kukamilisha mpango kazi aliyopewa mkandarasi katika eneo hilo. Kazi hiyo, inatarajia kukamilika ifikapo mwezi Aprili, 2021.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa usambazaji wa umeme vijijini umekuwa unafanyika kwa awamu, vijiji vinne vilivyobaki ambavyo ni Kijiji vya Rumashi, Nyamtukuza, Nyabibuye na Kinyinya viko katika mpango wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili utakaoanza mwezi Februari 2021 na kukamilika Septemba, 2022.