Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali imekiri kabisa kwamba wananchi wa Tarime asilimia 20 ndiyo wanaopata maji. Tatizo la maji ni Tanzania nzima. Sasa napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa miradi ya muda mfupi; visima virefu, Mradi wa Bwawa la Nyanduma ambalo tumekuwa tukilitengea fedha lakini haziendi na miradi mingine kama ya Gamasala na kwingineko kwa Tarime Mji, napenda kujua, ni lini Serikali itaenda kuchimba vile visima 23 ambavyo wameahidi kuanzia mwaka 2016 viweze kuwa suluhisho la muda mfupi kwenye Kata ya Kitale, Nyandoto, Kenyamanyoli na Mkende wakati tunasubiria Mradi wa Ziwa Victoria? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, jana wakati wameweka Mpango hapa, Serikali imekiri kabisa kwamba imepeleka maji vijijini kwa asilimia 70.1, wamechimba visima miradi 1,423 ambapo kuna vituo…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Esther, naomba uulize swali tafadhali.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Miradi hiyo ina vituo 131,000. Kwa Rorya tuna mradi mkubwa kule Kirogo ambao umetumia zaidi ya shilingi bilioni 1.3, ulitakiwa kuwa na vituo 23…

NAIBU SPIKA: Swali Mheshimiwa.

MHE. ESTHER N. MATIKO: … lakini kuna vituo vitatu tu ambavyo vinatoa maji. Ni lini sasa Serikali itahakikisha maji yanatoka kule Kirogo kwa vituo vyote 23 na siyo vituo vitatu tu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wote wanapata maji safi, salama na ya kutosheleza kwa maeneo yote ya nchi yetu ya Tanzania. Hivi karibuni Mheshimiwa Waziri alikuwa ziarani hapo Tarime na aliweza kuwasiliana na kuambatana na Mbunge wa Tarime Mjini ambaye ni Mheshimiwa Kembaki na Mbunge wa Tarime Vijijini, Mheshimiwa Naibu Waziri Waitara na Mheshimiwa Waziri ametoa ahadi hivyo visima vyote vitachimbwa ndani ya kipindi hiki cha miaka mitano. Kwa kuanza, katika mwaka wa fedha ujao, visima vitachimbwa na maji safi na salama yatapatikana bombani kwa wananchi wote wa Tarime. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama nilivyojibu kwenye jibu langu la awali ambalo ni jibu langu la msingi. Eneo la Rorya visima hivi vitatu kwa sasa hivi vinapata maji kati ya 27. Vijiji hivi vinakwenda kupatiwa huduma kupitia Mwaka wa Fedha 2021/2022 lakini vile vile tayari Wahandisi wetu wa eneo lile wanaendelea na hii kazi na visima vile ambavyo vilisalia vinakwenda kuchimbwa na kuhakikisha kuona kwamba vinakwenda kutoa maji ya kutosheleza kwa wananchi wote wa Rorya.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa ziara yake aliyoifanya ndani ya Jimbo langu la Rorya ikiwa ni pamoja na maelekezo ya Mradi wa Kirogo kwamba mkandarasi aliyetekeleza ule mradi kwa kiwango cha chini achukuliwe hatua. Kwa hiyo, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa maamuzi makubwa na mazuri aliyoyafanya kipindi alipofanya ziara yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi huu wa maji unaotoka Ziwa Victoria kwenda Tarime unaanzia ndani ya Jimbo langu la Rorya, zaidi ya Kata 11 na vijiji zaidi ya 28 vinategemea kufaidika na mradi huu. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuanza kutekeleza mradi huu hata kama ni kwa awamu ili kutatua changamoto za mradi huo wa maji ambao kimsingi utashughulika na Jimbo la Rorya, Tarime Vijijini na Tarime Mjini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Serikali tumeweka mikakati kuhakikisha tunaondoa changamoto ya maji kwenye maeneo yote yenye shida hiyo. Kwa Jimbo la Rorya, napenda kumwambia Mheshimiwa Mbunge, tayari Wizara iko kwenye michanganuo ya kuleta fedha katika maeneo hayo. Vilevile nimwambie tu kwamba baada ya Bunge hili, fedha awamu hii inayofuata, Jimbo lake pia limezingatiwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa miaka mingi wananchi wa Jimbo la Handeni Mjini wamekuwa wakiishi katika dhiki kubwa ya maji. Ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji wa Handeni Trunk Main kutoka Mto Ruvu kwenda Handeni?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Napenda kumpongeza Naibu Waziri wangu kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, anayelala na mgonjwa ndiye anayejua mihemo ya mgonjwa. Mimi naishi Tanga, najua moja ya changamoto kubwa ni eneo la Handeni. Serikali imeainisha miji 28 na tumeshapata Dola milioni 500 kuhakikisha tunatatua tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa tuko katika hatua ya manunuzi. Ndani ya mwezi Aprili, Wakandarasi wote watakuwa site kuhakikisha tunajenga miradi mikubwa ya maji. Hii ni katika kutimiza azma ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kumtua mwanamama ndoo kichwani. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria umeshafika Mkoani Tabora. Jimbo la Tabora Mjini ni moja kati ya wanufaika wa mradi huo. Je, ni lini Serikali itaanza usambazaji wa maji katika Jimbo la Tabora Mjini ili wananchi wa maeneo ya pembezoni ambao hawana maji kabisa waweze kunufaika na mradi huu? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Moja ya ahadi kubwa sana kwa wananchi wa Tabora ni kuyatoa maji ya Ziwa Victoria na kuyaleta Tabora. Ni jambo kubwa ambalo amelifanya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na ahadi hiyo imetimia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ni wa zaidi ya shilingi bilioni 600, nasi kama Wizara mradi huu tumeukamilisha na tume-save zaidi ya shilingi bilioni 25. Fedha zile zilizobaki zote zitatumika kwa ajili ya usambazaji wa maji, wananchi wote ambao hawana maji katika Mkoa wa Tabora wataweza kupata huduma ya maji. Kazi hiyo imekwishaanza na wakandarasi wako site kwa ajili ya uendelezaji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Rwakajunju ulioko Karagwe, nimeshauliza sana maswali katika Bunge la Kumi na Moja na mara zote huwa najibiwa kwamba mradi huo utatekeleza hivi karibuni lakini hadi sasa bado haujatekelezwa. Nini majibu ya Serikali kuhusu mradi huu ili kuwatua ndoo akina mama wa Karagwe? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi huu utatekelezwa kwa awamu katika mwaka wa fedha wa 2021/2022.