Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 78 2021-02-09

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER NI. MATIKO Aliuliza:-

Je, ni lini Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Mji Mdogo wa Tarime wanapata huduma ya maji safi na salama kupitia Mradi wa Maji wa Mserereko Nyandulumo; visima vitatu Rebu, Jeshi la wokovu na Viambwi, na bwawa la maji Tangota. Vyanzo hivi vyote vinazalisha wastani wa lita 1,200 kwa siku wakati jumla ya mahitaji ni lita 6,000 za maji kwa siku. Utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria utaweza kuhudumia maeneo yote ya mji wa Tarime kwa kuzalisha wastani wa lita 6,500 kwa siku ambazo ni zaidi ya mahitaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Tarime, Serikali imepata mkopo kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim jumla ya Dola za Marekani millioni 500 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika miji 28 ya Tanzania Bara na Zanzibar. Moja ya miji itakayonufaika na mkopo huo ni Mji wa Tarime ambao utatumia chanzo cha Ziwa Victoria. Kwa sasa mradi upo katika hatua za manunuzi ya wakandarasi wanaotarajiwa kuwepo eneo la mradi ifikapo mwezi Aprili, 2021 na ujenzi wa mradi unatarajiwa kuchukua miezi 24.