Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Mpepai na Lipilipili?

Supplementary Question 1

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa chanzo cha umeme cha maji cha Tulila kipo katika Kata ya Mpepai na miundombinu yake inapitia katika Kitongoji cha elfu mbili na vijiji vya Kata za Mapendano kuelekea Songea, Serikali haioni umuhimu wa kuvipatia Vijiji vya Kata za Mpepai na Kihungu umeme kwanza kabla ya vijiji vingine hasa ukizingatia vijiji hivyo hulinda na kuitunza miundombinu hiyo na hivyo kuwafanya wananchi wa Mpepai kupata hisia za kuwa wametengwa na kubaguliwa kwenye huduma hiyo ya umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ni kweli miundombinu ya umeme kutoka katika chanzo cha maji cha Tulila inapita katika Kata za Mpepai na Kihungu. Katika Kata ya Kihungu kuna Vijiji vya Pachasita na Kihungu ambavyo tayari vimeunganishwa na huduma ya umeme. Kijiji kimoja cha Lipembe kitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III unaoendelea.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika jibu la msingi kuwa kupitia utekelezaji wa mradi wa REA III, Mzunguko wa pili, vijiji vyote vya Kata ya Mpepai ambavyo ni Lipilipili, Luhangai, Mtua, Mpepai na Ruvuma chini vitapatiwa umeme.