Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 7 2020-03-31

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Mpepai na Lipilipili?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sixtus Raphael Mapunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa kusambaza umeme vijijini katika vijiji vyote vya Tanzania Bara. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2021. Mradi wa REA III unaoendelea utapeleka umeme katika vijiji 50 vya Wilaya ya Mbinga kupitia Mkandarasi Namis Corporate Ltd anayetekeleza kazi hiyo katika Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Mpepai na Lipilipili pamoja na vijiji vingine vilivyobaki katika Wilaya ya Mbinga vitapatiwa umeme kupitia Mradi unaoendelea. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vya Mpepai na Lipilipili inahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 18, ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 22, ufungaji wa transfoma nane za KVA 50, 100 na 200, pamoja na kuwaunganishia huduma ya umeme wateja wa awali 313. Gharama ya mradi ni shilingi milioni 977.