Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE (K.n.y. MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akikemea sana baadhi ya kodi ambazo zimekuwa ni kero kwa wananchi:- Je, ni kwa nini baadhi ya Halmashauri zimekuwa zikikaidi agizo hilo la Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru sana kwa majibu ya Serikali, hata hivyo nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, Ofisi ya Rais, TAMISEMI haiwezi ikatoa waraka kwa halmashauri zetu zote nchini ikiainisha kodi zote za kero ambazo zilifutwa na Bunge hili? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vitambulisho vya wajasiriamali pamoja na nia njema iliyo nyuma yake, utekelezaji wake bado ni kero kubwa nchini. Je, Serikali pia haiwezi ikatoa maelekezo ya jinsi ya kutekeleza zoezi hilo ili tuwe na usare nchi nzima kuliko hali ilivyo sasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, anauliza kama Serikali inaweza ikatoa waraka ambao unaainisha kodi za kero ambazo zilifutwa na Bunge hili Tukufu.

Naomba tupokee ushauri huo na naomba niahidi kwamba waraka huu utatengenezwa na utasambazwa nchi nzima na Waheshimiwa Wabunge watapata nakala wa kuonesha kodi ambazo ni kero zilizofutwa na Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza habari ya vitambulisho vya wajasiliamali. Ni kweli kama ambavyo wewe mwenyewe umeongezea, nilitoa tamko la Serikali katika Bunge hili Tukufu ulinipa fursa hiyo, lakini vilevile pamoja na waraka wetu ambao umetolewa nchi nzima na maelezo uliyotoa mara kadhaa katika Bunge hili, bado inaonesha kuna changamoto katika utekelezaji wa jambo hili.

Mheshimiwa Spika, tulisema tunapoanza 1st July, mwaka wa fedha mpya wa 2019/2020, tutatoa waraka mahsusi na Waheshimiwa Wabunge watapata nakala ukianisha nani anapaswa kutozwa kodi ya wajasiriamali na nani anapaswa kupewa kitambulisho. Kwa kweli baada ya kutoa waraka huo, wale wote ambao watakiuka wakaienda kinyume na maelekezo haya ambayo kimsingi siyo matamanio ya Serikali na siyo matakwa ya Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Rais alimaanisha kuwasaidia wajasiriamali wadogowadogo wasipate usumbufu mtaani kwao wanapofanya biashara ndogondogo ya kujikimu kutozwa kodi kubwa na watu wa TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge na Watanzania waendelee kuvuta subira, jambo hili tunalifanyia kazi na kwa kweli baada ya hapo itakuwa ni utekelezaji, hakutakuwa na msalia Mtume. Watu wote wafanye shughuli zao bila kuvunja sheria lakini wasipate bughudha ambazo kwa kweli ni kero. Ahsante. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE (K.n.y. MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE) aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akikemea sana baadhi ya kodi ambazo zimekuwa ni kero kwa wananchi:- Je, ni kwa nini baadhi ya Halmashauri zimekuwa zikikaidi agizo hilo la Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Ninavyofahamu mimi, service levy haichajiwi kwa mfanyabiashara mmoja ambaye amefungua duka lake na amelipa leseni na kodi ya mapato, lakini wafanyabiashara wadogowadogo kwenye baadhi ya Halmashauri wanachajiwa service levy, nini kauli ya Serikali juu ya hili?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pauline Gekul, Mbunge wa Babati Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli, ulipaji wa kodi ni kwa mujibu wa sheria na taratibu na sheria zipo na wasimamizi wanatakiwa kufuata taratibu hizo. Sasa Mheshimiwa Mbunge kama kuna maeneo ambayo watu wanachanganya analipa service levy ambayo imeelekezwa na bado anatozwa kodi nyingine, nafikiri tupate maelekezo yake na taarifa muhimu tuweze kulifanyia kazi.

Hata hivyo, kodi italipwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na sheria ipo, tunaomba hao wote wanaosimamia jambo hili watende haki na wasikilize watu na kutoa elimu ya umma. Ahsante.