Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 449 2019-06-25

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE (K.n.y. MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE) aliuliza:-

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akikemea sana baadhi ya kodi ambazo zimekuwa ni kero kwa wananchi:-

Je, ni kwa nini baadhi ya Halmashauri zimekuwa zikikaidi agizo hilo la Mheshimiwa Rais?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe, Mbunge wa Kavuu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kodi kero zilifutwa na Serikali kupitia marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290 mwaka 2017. Hivyo, Halmashauri yoyote inayoendelea kuwatoza wananchi kodi ambazo zilifutwa na Serikali kwa mujibu wa sheria ni kukiuka maelekezo ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, natumia fursa hii kuziagiza Halmashauri kuacha kutoza kodi ambazo zimefutwa kwa mujibu wa sheria. Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitasita kuchukua hatua za kisheria kwa Halmashauri ambayo itabainika kuwatoza wananchi kodi ambazo zimefutwa kwa mujibu wa sheria. Aidha, endapo Mheshimiwa Mbunge anazo taarifa za Halmashauri inayotoza kodi zilizofutwa, tunaomba taarifa hizo ili Seriali iweze kuchukua hatua. Ahsante.