Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Je, ni watalii wangapi walitembelea Kisiwa cha Mafia kwa mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 1

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri isipokuwa nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, pamoja na uzuri na vivutio vyote hivi vya utalii alivyovisema Mheshimiwa Naibu Waziri, Kisiwa cha Mafia hakijawahi kuonekana kwenye channel ya utalii inayoonyeshwa katika Azam. Sasa je, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri atawaelekeza wahusika wa vipindi hivyo waje kufanya shooting pale Mafia na vivutio vile viweze kuonekana?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri anasema Serikali inajitahidi kuimarisha miundombinu ya kuingilika Mafia ili kuweza kupata watalii wengi zaidi. Tunaishukuru Serikali imetupatia boti ile ya DMI ambayo kwa sasa inamaliziwa matengenezo pale, lakini imekwama kupata kibali cha TASAC kutokana na matatizo ya hitilafu za kiufundi na kuna matatizo ya kibajeti ya Chuo cha DMI.

SPIKA: Swali Mheshimiwa?

MHE. MBARAKA K. DAU: Je, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mtaweza kuwasiadia Chuo cha DMI matatizo yao ya kibajeti ili waweze ili waweze kulipia boti ile na iweze kuja Mafia?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba lengo la kuanzishwa kwa channel ya utalii ni kuhakikisha kwamba inatangaza vivutio mbalimbali vilivyopo katika nchi yetu katika maeneo yote na maeneo hayo ni pamoja na Kisiwa cha Mafia. Lakini naomba nikiri kwamba channel hii imeanzishwa tu, haina muda mrefu na uandaaji wa vipindi hivi ni unahitaji gharama na pesa nyingi na nchi yetu ni kubwa, bado hatujamaliza kuandaa vipindi, lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kisiwa hiki ni maeneo yetu ya kimkakati ambayo tumeyaweka kwa ajili ya kuhamasisha utalii na nimechukua pamoja na maombi yake lakini ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba watu wetu wanaoandaa vipindi kupitia TBC wanakwenda katika eneo hili kuvitambua na kuvirekodi vivutio vyote vya utalii na kuvitangaza.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na kwamba haijaonekana tutahakikisha kwamba tunatoa maelekezo kisiwa hiki kiweze kupewa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, kwanza naomba nimshukuru kwa kuipongeza Serikali kuboresha miundombinu mbalimbali hasa uwanja wa ndege ambao Mheshimiwa Mbunge amesahau kusema kuna uwanja wa ndege bora kabisa pale Mafia na nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba boti hii ambayo imekwama kwa masharti machache pale DMI nitashirikiana na wenzangu wa Wizara ya Uchukuzi kuhakikisha kwamba taratibu zinakamilishwa ili boti hii iweze kuanza kutoa huduma na kupeleka watalii katika Kisiwa cha Mafia, ahsante sana.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Je, ni watalii wangapi walitembelea Kisiwa cha Mafia kwa mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 2

MHE.DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Kisiwa hichi cha Mafia ni eneo nyeti sana sio tu kwa ajili ya shughuli za utalii bali pia ni eneo ambalo linatulishia samaki, mazalia ya samaki katika bahari yetu. Sasa kwa kuwa ni kisiwa kiko strategic Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa nini sasa isikae na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na TAMISEMI kuleta mkakati mahususi wa kuwezesha shughuli za wananchi katika maeneo haya ya Mafia ambao wako duni sana na majority ni wavuvi, wainuliwe kiuchumi na kuweza kuinua utalii pamoja na shughuli za uvuvi ili kuinua zaidi uchumi wetu kwa ujumla nchini?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba maeneo ya Kisiwa hiki cha Mafia ni maeneo ambapo kwanza kuna visiwa vingi, lakini maeneo yenye wavuvi wengi, lakini ni maeneo ya mazalia ya samaki na baadhi ya maeneo haya ambayo nimeyataja kwamba yako chini ya marine park ni maeneo yanayohifadhiwa kwa ajili ya mazalia ya samaki pia ndipo ambapo utalii wa kuzamia majini unafanyika na ndipo ambapo kuna akiba ya under water cultural heritage nyingi ambazo ziko maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu suala hili ni cross cutting linahitaji pengine kujadiliwa na wizara nyingi mbalimbali. Tumechukua wazo lake lakini nimhakikishie kwamba mpaka wavuvi na wananchi katika maeneo hayo wanaandaliwa vizuri ili kuhakikisha kwamba wanafaidika na uwepo wa shuguli za uvuvi pia na uwepo wa shughuli za utalii katika maeneo hayo.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Je, ni watalii wangapi walitembelea Kisiwa cha Mafia kwa mwaka 2017/2018?

Supplementary Question 3

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa uwepo wa mamba pia ni sehemu ya kivutio kwa watalii lakini kutokana na ongezeko kubwa sana mazalio ya mamba katika Mto Ruvuma na kuleta athari kubwa sana kwa wananchi.

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuja kwenye Jimbo langu kuona athari kubwa zinazojitokeza na kutafuta changamoto za kutatua tatizo hilo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba limekuwepo ongezeko kubwa sana la mamba katika maeneo yetu mengi mamba, boko na wanyama wengine ambao hawatumiki moja kwa moja sana na kuhamasisha utalii na katika eneo hili la Mto Ruvuma ambalo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akisema wamesababisha shughuli za uvuvi na shughuli za matumizi ya maji ya kawaida ya Mto Ruvuma kushindikana.

Mheshimiwa Spika, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyomjibu hivi karibuni kwenye swali lake la msingi kwanza tulielekezwa watu wetu wa TAWA kuhakikisha kwamba wanapeleka visima vya maji karibu katika vijiji ambavyo viko karibu na maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, pili, tuliwaagiza watu wetu wa TAWIRI kufanya utafiti na kutueleza mamba waliopo wamezidi kwa kiasi gani ili tuweze kuweka mkakati wa kuwavuna, lakini nimhakikishie pia Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari kwenda katika eneo hilo kwenda kuangalia hali halisi na kuzungumza na wananchi.