Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 47 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 393 2019-06-18

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:-

Je, ni watalii wangapi walitembelea Kisiwa cha Mafia kwa mwaka 2017/2018?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau, Mbunge wa Mafia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kisiwa cha Mafia ni moja ya eneo la kimkakati katika uendelezaji wa utalii wa fukwe nchini. Katika miaka ya karibuni kisiwa hicho kimekuwa kikitembelewa kwa wingi na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi. Wageni hao wamekuwa wakivutiwa na vivutio mbalimbali vinavyopatikana katika kisiwa hicho ikiwemo papa potwe, magofu ya kale, utamaduni wa fukwe nzuri. Aidha, watalii wamekuwa wakivutiwa na michezo ya kwenye maji (scuba diving, sport fishing and snorkelling) na kuongelea na samaki aina ya papa.

Mheshimiwa Spika, kutokana na uzuri wa Kisiwa cha Mafia idadi ya watlii wanaotembelea kisiwa hicho imeendelea kuongezeka ambapo katika mwaka 2017/2018 jumla ya watalii 5,412 walitembelea Kisiwa cha Mafia hususani katika Hifadhi yetu ya Bahari ya Hindi katika eneo la Kisiwa cha Mafia (Marine Park and Reserve-Mafia). Kati ya watalii Watanzania walikuwa 252 na wageni walikuwa 5,160. Idadi hii ya watalii waliotembelea Mafia ni sawa na ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa na watalii 4,817 waliotembelea kisiwa hicho katika msimu wa mwaka 2016/2017. Katika kuhakikisha kuwa Kisiwa cha Mafia kinafikika kwa urahisi, Serikali inaendelea na mikakati ya kuboresha miundombinu ya kisiwa hicho ikiwa ni pamoja na kujenga meli na kuboresha maegesho ya meli katika Bandari ya Nyamisati na Mafia.

Mheshimiwa Spika, namsihi Mheshimiwa Mbunge aunganishe nguvu kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya umma na binafsi wa Wilaya ili kuboresha miundombinu itakayosaidia kukuza sekta ya utalii katika Kisiwa cha Mafia kukitangaza zaidi ndani na nje ya nchi na kuhamasisha uwekezaji.