Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kwamba Serikali ni pamoja na Serikali za Mitaa na mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka kwa niaba ya Serikali au Halmashauri. Je, kwa nini katika kipindi chote cha uwepo wa Katiba hiyo Serikali haijatunga Sera ya Ugatuaji Madaraka ambayo ingewezesha kuweka mfumo wa kisheria unaoelekeza mipaka, majukumu na utaratibu wa utekelezaji wa matakwa hayo ya Kikatiba?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na utaratibu ambao ni kinyume cha Sheria Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Makatibu Tarafa na hata Watendaji wa Kata kuwafukuza Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji papo kwa papo kwenye mikutano ya hadhara.

Je, Serikali ina tamko gani kuhusu jambo hili ambalo ni kinyume cha sheria? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wamekuwa wakifanya kazi kubwa sana wakiwasaidia Madiwani na Wabunge na kwa kweli ndiko Serikali za wananchi ziliko, lakini wamekuwa hawapati posho, posho zao zinasuasua, hawapati mishahara, wamekuwa wakifanya kazi kwa taabu sana.

Je, Serikali inasema nini hasa katika hiki kipindi cha Bajeti kuhakikisha kwamba watu hawa wamepata posho kidogo kwa ajili ya kuwasaidia kufanya kazi zao kwa ufanisi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba ni-declare interest kwamba na mimi pia kuanzia mwaka 2014 hadi 2017 nilikuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule, Ukonga - Dar es Salaam, swali lake la kwanza anaulizia juu ya namna ambavyo Wenyeviti wa Vijiji Vitongoji na Mitaa wanavyoondolewa madarakani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa sheria, kwanza kama unataka kumuondoa Mwenyekiti wa Kijiji, hayo maeneo niliyoyataja, la kwanza ni lazima wapatikane watu ambao wana watuhumu hao viongozi katika eneo lao la kiongozi ambalo wamechaguliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili lazima hao watu waandike malalamiko kwa maandishi wampelekee Mkuu wa Wilaya wakitaja tuhuma moja baada ya nyingine ambayo muhusika na mlalamikiwa ametenda na jambo la tatu ni lazima Mkuu wa Wilaya au anayehusika ataandika maana yake sheria inamtambua Mkuu wa Wilaya kwenye ngazi ya Wenyeviti wa Vijiji kuja chini, atamwandikia Mwenyekiti wa Kijiji, Kitongoji au Mtaa tuhuma zake kwa maandishi, ndani ya muda usiozidi siku saba mtuhumiwa atalazimika kujibu tuhuma alizopewa na baada ya hapo, baada ya kupokea majibu ya tuhuma zile Mkuu wa Wilaya ataitisha mkutano wa wananchi wa eneo husika na sheria inasema watakao hudhuria siyo chini ya nusu ya wakazi wa eneo husika na wawe wamekuwa registered kwenye registration ya mtaa husika wanaotambulika, watu wazima wenye akili timamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo watapewa nafasi ya kujitetea mbele ya mkutano huo, atasomewa tuhuma zake, atapewa nafasi ya kujitetea na baada ya hapo wananchi baada ya kumsikiliza watapiga kura sasa kuonesha kwamba hawamtaki, mbili ya tatu (2/3) ya mkutano uliohudhuriwa wakikubali kwamba hafai ataondolewa madarakani na huo ndiyo utaratibu na naomba viongozi wazingatie muongozo huo wa kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni habari ya posho au mishahara kwa Wenyeviti wa Mitaa, Vitongoji na Vijiji. Swali hili nimejibu mara nyingi, naomba nirudie; kwa mujibu wa sheria hizi kazi, zetu hizi, Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji hawapewi mishahara, lakini hata hivyo kwa sababu ya kuangalia umuhimu wa shughuli ambazo wanafanya na unyeti na ni kweli wanafanya kazi zaidi ya masaa 24 sheria imeelekeza na TAMISEMI tumeelekeza, naomba nielekeze pia kulingana na mapato ya Halmashauri kwenye eneo husika Wakurugenzi wetu wamekuwa wakipanga namna ya kuwapa posho za kujikimu, kuweza kulipia ofisi zao, kuwapa vitendea kazi ikiwepo na photocopy. Maeneo mengine kulingana na mapato yao wamepanga wanalipwa shilingi 50,000 kwa mwezi, kule Dar es Salaam najua wanalipwa shilingi 100,000 kwa mwezi, kwa hiyo, inategemea na mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sheria haijabadilishwa na Waheshimiwa Wabunge Bajeti ya TAMISEMI imeshapitishwa na kwa kweli hatukupokea maoni yoyote ya Halmashauri wakitaka kupandisha posho za Wenyeviti wa Mitaa au wa Vijiji, hili jambo tulipokee, tutafakari kwa pamoja tukipata uwezo tuboreshe utaratibu huu ili Wenyeviti wa Mitaa waweze kulipwa kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya, wanatusaidia sana katika kazi hii na wanafanya kazi ya kipolisi, mahakama, kifamilia na mambo mengi kadha wa kadha ambayo yanafanyika. Ahsante. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kwamba Serikali ni pamoja na Serikali za Mitaa na mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka kwa niaba ya Serikali au Halmashauri. Je, kwa nini katika kipindi chote cha uwepo wa Katiba hiyo Serikali haijatunga Sera ya Ugatuaji Madaraka ambayo ingewezesha kuweka mfumo wa kisheria unaoelekeza mipaka, majukumu na utaratibu wa utekelezaji wa matakwa hayo ya Kikatiba?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amejibu mimi kwanza nimpongeze kwa majibu yake mazuri, lakini bado kuna tatizo la hawa watendaji wetu yaani kwa maana kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Madiwani ni kwamba hawajapata semina, pamoja na kwamba sheria/sera bado haijaletwa ya ugatuzi wa madaraka lakini bado uko umuhimu wa kuwapa semina mara kwa mara ili waweze kujua mipaka yao ili waweze kuboresha utendaji wao wa kazi.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa semina hawa watu, Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji ili waweze kufanya kazi vizuri? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, inawezekana kuna maeneo hawa viongozi hawajapata semina lakini ninachojua na maelekezo ya TAMISEMI ambayo na mimi nimesema nilikuwa Mwenyekiti wa Mtaa tulifanyiwa baada ya uchaguzi wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa wale viongozi wakishapatikana kabla ya kuanza kazi wanapewa semina ikiwa ni pamoja na kuapishwa, hawa wajumbe wanakula viapo vya uaminifu kwenye ngazi ya Halmashauri na wanapaswa kuapishwa na Mwanasheria Mkuu wa Halmashauri husika, hilo linapaswa kufanyika, kama kuna mahali halikufanyika nitaomba kwa sababu tunaenda kwenye uchaguzi wa mwaka huu tutalisimamia ili viongozi wakishapatikana wapate semina, waapishwe lakini kubwa zaidi ni lazima wajue mipaka yao ya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako majukumu na kuna tofauti kubwa kwa mfano ya Wenyeviti wa Mitaa na Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Mitaa ni waratibu wa shughuli za Serikali za Mitaa, wakati Wenyeviti wa Vijiji ni Serikali kamili wana maamuzi wanaweza hata wakachukua rasilimali za eneo fulani wakauza wakafanya miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hayo mambo tutayasimamia ili yaweze kufanyiwa kazi na naomba viongozi wetu wa Halmashauri na Mikoa wajipange, baada tu ya uchaguzi haitakiwi Mjumbe wa Serikali ya Mtaa au wa Kijiji au Mwenyekiti aanze majukumu yake bila semina, kiapo na mafunzo tutayazingatia na chuo chetu kikuu cha mafunzo ya Serikali za Mitaa za Hombolo kina nafasi hiyo na hata nyie Waheshimiwa Wabunge mnakaribishwa hata sasa mkitaka na wajumbe wenu mnawapeleka pale, tuna nafasi ya kutosha walimu waliobobea, karibu Hombolo Chuo cha Serikali za Mitaa wapate mafunzo ili wafanye kazi kwa kuboresha huduma za kijamii. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kwamba Serikali ni pamoja na Serikali za Mitaa na mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka kwa niaba ya Serikali au Halmashauri. Je, kwa nini katika kipindi chote cha uwepo wa Katiba hiyo Serikali haijatunga Sera ya Ugatuaji Madaraka ambayo ingewezesha kuweka mfumo wa kisheria unaoelekeza mipaka, majukumu na utaratibu wa utekelezaji wa matakwa hayo ya Kikatiba?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kuna baadhi ya Wenyeviti katika vijiji vyetu baada kuteuliwa tu baada ya miezi mitatu/minne wanajiuzulu wengine wanafariki, lakini hakuna chaguzi zinafanyika na mfano hasa kwenye Wilaya yangu kunakaa wazi, wanateuliwa tu mtu anakaimu anakuwa pale, sasa demokrasia inasemaje kuhusu watu wanaojiuzulu na wanaofariki kwa nini uchaguzi haufanyiki?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, inawezekana kweli, nimesikia sikia naomba nitoe maelekezo, kwanza, hakuna mtu anaitwa Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji, Kitongoji au Mtaa kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa, haipo hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika ni kwamba Wajumbe na kuna watu wengine mtu akijiuzulu anakaimu kwa muda mrefu na anatembea na muhuri kwamba ni Mwenyekiti, hilo zoezi kama lipo kuanzia sasa na leo muda huu, likome halipo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika mtu akijiuzulu Wajumbe wa Serikali ya Mtaa wanapokutana kwenye kikao, miongoni mwao anakuwa Mwenyekiti wa kikao hicho na uenyekiti wake unakoma mara tu baada ya kikao kuisha wakati ule, anayepaswa kufanya kazi ya kiutendaji ni Mtendaji wa Kijiji au Mtendaji wa Mtaa mpaka uchaguzi ufanyike, lakini uchaguzi wa Serikali za Mitaa, wakati wowote ikitokea gap tunategemea kupata taarifa kutoka ngazi ya Kijiji au Mtaa inakuja TAMISEMI, tunaruhusu wafanye uchaguzi kwa sababu kwanza unasimamiwa na eneo husika pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mtu akijiuzulu, kwa mfano mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi Mkuu kama sasa, hatukuruhusu kwa sababu sheria inazuia huu muda hauruhusiwi, lakini muda wowote wa nyuma Mheshimiwa Ally Keissy kama ilitokea ni bahati mbaya sana na tunaisimamia tupate taarifa baada ya uchaguzi huu, kama inatokea mtu amejiuzulu baada ya muda siyo mrefu sana inabidi achaguliwe ili wananchi wahudumiwe na mtu ambaye wamempigia kura, waweze kumwajibisha kwa ile imani waliyompa. Ukikaimisha mtu ambaye hawakumchagua wao watashindwa kumwajibisha na ukienda kumuhoji anasema mimi siyo Mwenyekiti nilikuwa nakaimu na anakimbia majukumu yake. Ahsante. (Makofi)