Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 355 2019-06-11

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:-

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kwamba Serikali ni pamoja na Serikali za Mitaa na mtu yeyote anayetekeleza madaraka au mamlaka kwa niaba ya Serikali au Halmashauri.

Je, kwa nini katika kipindi chote cha uwepo wa Katiba hiyo Serikali haijatunga Sera ya Ugatuaji Madaraka ambayo ingewezesha kuweka mfumo wa kisheria unaoelekeza mipaka, majukumu na utaratibu wa utekelezaji wa matakwa hayo ya Kikatiba?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Jimbo la Mchinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali za Mitaa zipo kwa mujibu wa Ibara ya 145 na 146 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Mwaka 1998 Serikali iliandaa andiko la kisera la maboresho ya Serikali za Mitaa ambalo ndio mwongozo wa utekelezaji wa Sera ya Ugatuzi wa Madaraka nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hata hivyo, kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho za kuandaa Sera ya Taifa ya Ugatuzi wa Madaraka ambayo inatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika katika mwaka wa fedha 2019/2020. Sera hiyo itaweka mfumo wa kisheria unaoelekeza majukumu na mipaka ya wadau mbalimbali kwenye utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika utoaji wa huduma kwa wananchi, ahsante.