Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. SAED A. KUBENEA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA) aliuliza:- Bado tatizo la kupungua na kukatika kwa umeme bado linaendelea na baadhi ya maeneo hayajafikishiwa umeme mpaka sasa. (a) Je, ni kwanini matatizo ya kukatika au kupungua kwa umeme katika Jimbo la Kibamba halijapatiwa ufumbuzi kinyume na Serikali ilivyoahidi? (b) Je, ni maeneo gani katika Jimbo la Kibamba mpaka sasa TANESCO haijafikisha umeme na lini yatafikiwa? (c) Je, kuna mkakati gani wa kupunguza gharama za wananchi kuunganisha umeme au kuwarejeshea wanapovuta wenyewe umbali mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoka na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utekelezaji wa miundombinu ya Dar es Salaam na ukatikaji wa umeme, TANESCO imekuwa haitoi taarifa ya kuwepo kwa tatizo la ukatikaji wa umeme katika baadhi ya maeneo ambayo miundombinu hiyo inatekelezwa, jambo ambalo linasabisha kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi wanaotumia umeme, lakini hasa katika maeneo ya umma, ikiwemo hospitali ya Sinza Jijini Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kwamba miundombinu ya TANESCO haiathiriki ya umeme kutokana na utengenezaji wa barabara zinazotengenezwa katika eneo hilo la Dar es Salaam?

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam, ambayo hayapati umeme wa kutosha, ni pamoja na katika Jimbo la Mheshimiwa Mwita Mwaikwabe Waitara, Jimbo la Ukonga, Mheshimiwa Ndugulile Jimbo la Kigamboni, Mheshimiwa Kubenea mwenyewe Jimbo la Ubungo na Majimbi mengine likiwemo la Kibamba.

Sasa Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam, ambalo ndiyo kitovu cha biashara, linapata umeme wa kutosha na wakati wote bila usumbufu wowote na hasa ukizingatia kwamba, mradi mkubwa wa umeme wa gesi uko Kinyerezi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Kubenea ameulizia taarifa, endapo, pindi umeme unapokatikatika. Nataka nimtaarifa Mheshimiwa Kubenea, kwamba Serikali kupitia TANESCO tulitoa maelekezo ya kutumia maendeleo ya teknolojia katika kuhakikisha wananchi inawafikia taarifa haraka na maendeleo hayo ni kupitia pia uundwaji wa ma-group mbalimbali na katika Mkoa wa Dar es Salaam, Kanda zote zimeundiwa ma-group na hata mimi mwenyewe nipo kwenye group la Kibamba la utoaji taarifa za huduma ya TANESCO na mikoa yeto ina ma-group ya whatsapp.

Mheshimiwa Naibu Spika, na sambamba na hilo pia, hata katika kikao cha maafisa habari nchi nzima kilichofanyika Mwanza, Shirika la Umme TANESCO na Wizara ya Nishati ni miongoni mwa taasisi na Wizara zilizofanya vizuri katika kuwahabarisha wananchi taarifa mbalimbali zinazohusiana na sekta ya nishati. Kwa hiyo, nataka niwape, pengine kama Mheshimiwa Mbunge hajaungwa kwenye haya ma-group nataka nielekeze kwamba Mbunge wa Ubungo sambamba na Wabunge wengine wote waungwe kwenye ma-group na viongozi wote ili iwe kiungo katika kutoa taarifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ameulizia namna ya uboreshaji wa miundombinu ya usafiri wa umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Kubenea, katika Mkoa wa Dar es Salaam, kwanza kuna mradi mkubwa wa upanuzi wa Kituo cha Ubungo, kituo hiki kinapokea umeme kutoka mitambo ya Kidatu kwa msongo wa kilo vote 220 na inapoza kwenye mashine za MVA 125 na inafanya kwamba, megawatts 200 kusambaza katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo, kituo hiki kinapokea umeme kutoka mitambo ya SONGAS megawatts 189, mitambo ya Ubungo ll megawatts 129 na Kituo cha Tegeta megawatts 45. Mahitaji ya Mkoa wa Dar es Salaam ni megawatts 500, lakini Kituo cha Ubungo kina uwezo wa megawatts 655. Lakini lazima niseme kwamba mitambo hii inafanyiwa ukarabati, wakati mwingine inafikia ukomo, inatakiwa ibadilishwe vipuli, kwa hiyo, inapotokea hiyo, ndiyo maana changamoto ya kukatikakatika umeme kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya nini? Serikali ya awamu ya tano kupitia TANESCO inaendelea na upanuzi wa Kituo cha Ubungo, imeshaagzia na imefika mashine ya MVA 300 ambayo itaongeza megawatts 240 kwenye msongo wa kilovoti 132 na kufanya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa na upatikanaji mkubwa wa megawatts za kutosha kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ameyataja Majimbo ya Ukonga, ametaja Jimbo la Kigamboni, kwamba lina changamoto. Nataka nimtaarifu, Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo haya, akiwemo Mheshimiwa Waitara, Mheshimiwa Ndugulile, wamefanya jitihada kubwa ya kufuatilia maeneo ambayo hayana umeme na ndiyo maana Serikali ikabuni mradi wa Peri-urban na imetenga bilioni 86 na sasa hivi hatua iliyokuwepo ile mikataba ya wakabdarasi ilishafikishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwa hiyo, niwatoe hofu wakazi wa maeneo ya Ukonga, ambako mimi mwenyewe nimefanya ziara kata sita, ikiwemo Zingiziwa, Buyuni, Kivule, lakini pia maeneo ya Somangila, maeneo ya Pembamnazi, maeneo ya Kisarawe ll, maeneo ya Msonga, maeneo ya Buyuni, yote hayo yametengewa bajeti na mradi utafanyika na kwa gharama za REA elfu 27. Wakazi wa Dar es Salaam wakae mkao wa tayari, Serikali ya Chama cha Mapinduzi imejipanga kutekeleza miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. SAED A. KUBENEA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA) aliuliza:- Bado tatizo la kupungua na kukatika kwa umeme bado linaendelea na baadhi ya maeneo hayajafikishiwa umeme mpaka sasa. (a) Je, ni kwanini matatizo ya kukatika au kupungua kwa umeme katika Jimbo la Kibamba halijapatiwa ufumbuzi kinyume na Serikali ilivyoahidi? (b) Je, ni maeneo gani katika Jimbo la Kibamba mpaka sasa TANESCO haijafikisha umeme na lini yatafikiwa? (c) Je, kuna mkakati gani wa kupunguza gharama za wananchi kuunganisha umeme au kuwarejeshea wanapovuta wenyewe umbali mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la ngongeza.

Tatizo la umeme lililopo Kibamba linafanana kabisa na tatizo la umeme lililopo katika Jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Tuna vijiji 22 havina umeme, lakini tangu Januari, 2019 mkandarasi wa REA amesambaza umeme katika vijiji viwili kwenye vijiji hivyo viwili amesambaza kitongoji kimojakimoja. Kwa hiyo, nini kauli ya Serikali sasa kuhakikisha kwamba hivi vijiji 22 vinapelekewa umeme na kuhakikisha kwamba mkandarasi huyu anasambaza umeme kwa kasi ili vijiji vyote 22 viweze kupata umeme? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hongoli atakuwa shahidi, tulifanya ziara pamoja naye katika jimbo lake na nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini nataka nimthibitishie mkandarasi JV Mufindi anaendelea na kazi, lakini nataka niwathibitishie Wabunge wote kwa sababu yapo maswali mengi ya Mradi wa REA, kwamba Mradi wa REA bado mudo upo, inatarajiwa ikamilike Juni, 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama Wizara Mhesimiwa Waziri wa Nishati ametoa maelekezo, miradi ikamilike ifikapo Septemba, 2019. Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kumsimamia mkandarsi kwa karibu na ukizingatia sasa hivi wakandarasi karibu wote wameshafanikiwa kupata vifaa vyote vya mradi. Kwa hiyo, nimtoe hofu tu kwamba vijiji 22 vitakalika na kasha tutaanza tena REA Awamu ya III mzunguko wa pili kwa vijiji vyake vyote vilivyosalia, ili kulifanya jimbo lake ifikapo 2021 yote iwe imemeremeta. Ahsante sana.