Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 35 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 295 2019-05-24

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. SAED A. KUBENEA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA) aliuliza:-

Bado tatizo la kupungua na kukatika kwa umeme bado linaendelea na baadhi ya maeneo hayajafikishiwa umeme mpaka sasa.

(a) Je, ni kwanini matatizo ya kukatika au kupungua kwa umeme katika Jimbo la Kibamba halijapatiwa ufumbuzi kinyume na Serikali ilivyoahidi?

(b) Je, ni maeneo gani katika Jimbo la Kibamba mpaka sasa TANESCO haijafikisha umeme na lini yatafikiwa?

(c) Je, kuna mkakati gani wa kupunguza gharama za wananchi kuunganisha umeme au kuwarejeshea wanapovuta wenyewe umbali mrefu?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa John John Mnyika, Mbunge wa Kibamba lenye sehemu (a) (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la kukatika kwa umeme katika Jimbo la Kibamba linatokana na zoezi la kuhamisha miundombinu ya umeme ili kupisha upanuzi wa barabara ya Dar es Salaam - Morogoro. Kwa sasa tatizo hilo limepungua, baada ya zoezi hilo kukamilika kwa asilimia 97 na itakamilika mapema mwezi Juni, 2019. Hali ya upatikanji wa umeme katika Jimbo la Kibamba imeimalika kutokana na kukamilika kwa kazi ya kubadilisha nguzo mbovu na kukata miti kwenye mkuza wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 kutoka Ubungo hadi Kibamba. Vilevile kupitia TANESCO imetenga shilingi bilioni 5 kwenye bajeti ya 2018/19 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Mloganzila, Luguruni, chenye uwezo wa MVA 90, kituo hiki kitasambza umeme katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kibamba, ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Mloganzila na hivyo kutatua tatizo la ongezeko la mahitaji ya umeme katika Jimbo la Kibamba.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Kibamba kuna baadhi ya maeneo ya ambayo hayajapatiwa huduma ya umeme ikiwa ni pamoja na maeneo ya Kibesa, Kisopwa, Kipera, King’azi, Msumi na baadhi ya maeneo ya Mpigi na Kwembe. Katika bajeti ya mwaka TANESCO ilienga shilingi bilioni 3.78 kwa ajili ya kupeleka umeme katika maeneo ya Kwembe kwa Tendwa, Kwembe Kipera, Mbezi Luis, Kibwegere, Msakuzi, Mpigi CCM ya Zamani, Kibamba Delini, Mpiji, Kwembe, Msumi na King’azi. Kazi ya kupeleka umeme katika maeneo haya inaendelea na itakamilika mwezi Septemba, 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yaliyosalia ya Kibesa, Kisopwa na Kipera, yatapatiwa umeme kupitia bajeti ya 2019/20.

(c) Mheshimiwa Naibu Spika, Mwezi Desemba, 2013, Serikali kupitia EWURA ilipunguza gharama za kuunganisha umeme kutoka shilingi 385,682, hadi 272,000 kwa wateja wa njia moja wa mjini, aliye ndani ya mita 30 ikiwa ni punguzo la asilimia 30. Kanuni za Sheria ya Umeme Kifungu 131 ya mwaka 2008 zilizotangazwa katika gazeti la Serikali Na. 63 la Tarehe 4 Februari, 2011 zinaelekeza TANESCO na mteja kukubaliana namna ya kurejeshwa kwa gharama zilizotumika kujenga miundombinu ya umeme kama TANESCO haitakuwa na uwezo wa kibajeti kwa wakati huo kumfikishia mteja huduma ya umeme.