Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB N. MWAMWINDI aliuliza:- Katika kuboresha utalii katika Hifadhi ya Ruaha:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kiwango cha lami barabara iendayo Hifadhi ya Ruaha pamoja na kuimarisha miundombinu ya ndani ya Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Leo nasimama mara ya tatu katika Bunge lako Tukufu nikiikumbusha Serikali kuhusu barabara hii itokayo Iringa kwenda Ruaha National Park.

Mheshimiwa Spika, barabara hii urefu wake ni kilometa 104 na kama majibu ya Naibu Waziri alivyosema kwamba imetengenezwa kwa kiwango cha lami kilomita 14. Kwa masikitiko makubwa ninasikitika kwamba barabara hii kwa hizo kilomita 14 imejengwa na Marais wote wanne. Upembuzi yakinifu ulishafanyika na kila mwaka Serikali inapanga fedha za ujenzi wa barabara hii. Je, ni kwanini Serikali inapata kigugumizi kuikamilisha barabara hii?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, barabara zote za ndani ni mbovu na wakati wa masika ni mahandaki, kiasi kwamba upitaji wake na watalii wanapata shida inapunguza pato la Taifa. Swali ni lini Serikali itapanga pesa kwa ajili ya kutengeneza barabara hii? Ahsante sana.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza nakiri kwamba katika jibu langu la msingi nimesema tumekwisha jenga kilometa 14 kati ya kilometa 130 ambazo zipo katika barabara hiyo, na barabara hiyo tayari imekwisha fanyiwa upembuzi yakinifu. Mheshimiwa Mbunge anafahamu juhudi za kilometa 14 ambazo zimekwisha fanyika sio haba. Lakini anafahamu yeye ni mjumbe wa Kamati ya Maliasili, tumekuwa naye katika ziara juhudi za Wizara yetu katika kuhakikisha kwamba barabara hizo zinajengwa ni kubwa, nimuombe awe na imani na Serikali kama yalivyo maeneo mengine barabara hii itajengwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake kuhusu ubovu wa barabara zilizopo ndani ya Ruaha ni kweli, pamekuwa na tatizo la ubovu wa miundo mbinu mbalimbali katika hifadhi ya Ruaha. Lakini nimesema katika jibu la msingi tunao mradi mkubwa REGROW, ambao tayari tulikwisha saini mkataba na umeanza kutekelezwa, Barabara zote pamoja na miundo mbinu mingine katika hifadhi ya Ruaha imo katika mkataba huo.

Mheshimiwa Spika, na nimhakikishie kwamba wakati kutengeneza mkataba huo maeneo yote haya ambayo yamekuwa yakisababisha hifadhi hii kushindwa kutumika wakati wa masika yatakuwa yamefanyiwa matengenezo makubwa na moja ya eneo ambalo Wizara yetu imehakikisha kwamba inaipa kipaumbele kufungua utalii maeneo hayo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ninafahamu juhudi zake kubwa za kupingania utalii maeneo ya Mkoa wa Iringa na kusini kwa ujumla lakini nimhakishie kwamba Serikali inalitilia maanani suala hilo.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. ZAINAB N. MWAMWINDI aliuliza:- Katika kuboresha utalii katika Hifadhi ya Ruaha:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kiwango cha lami barabara iendayo Hifadhi ya Ruaha pamoja na kuimarisha miundombinu ya ndani ya Hifadhi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nashukuru katika hifadhi ya Ruaha tatizo sio barabara tu, hata Mto Ruaha mkuu ambao ndio kitovu cha hifadhi ya Ruaha, unatanuka na unakauka kwa baadhi ya vipindi hali ambayo inahatarisha maisha ya wanyama na inahatarisha hifadhi nzima yenyewe kutoweka kabisa. Sasa Serikali inachukua hatua gani kuona kwamba ule mto hautanuki na maji yanaendelea kutitirika katika kipindi cha mwaka mzima ili wanyama wetu waendelee kuhuika katika hifadhi ile?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli historia inaonyesha Mto Ruaha ulikuwa una flow maji yake kwa mwaka mzima na kwa miaka ya hivi karibuni umeendelea kuwa na tabia tofauti kwa maana unapoteza maji katika kipindi cha miezi miwili mpaka mitatu kwa mwaka. Lakini sababu zinafahamika ikiwemo pamoja na matatizo ya taabu ya nchi lakini pia matumizi makubwa yanayofanywa na wakulima walioko kwenye mabonde yaliyoko juu Mto Ruaha.

Mheshimiwa Spika, katika mradi wetu wa REGROW moja ya maeneo ambayo yanaenda kushughuliwa ni pamoja na elimu kubwa itakayotolewa kwa wakulima hao. Lakini miundombinu ambayo itatengezwa ili kuwafanya wanaotumia maji kwa ajili ya kilimo katika maeneo hayo iwe ni miundombinu ya kisasa ambayo itaruhusu flow ya maji kuendelea kuwepo, kuliko hivi sasa hivi wakulima wanazuia maji na kuyaweka kwenye mabwawa ya akiba kwa mwaka mzima hata kama maji hayo hawayatumii. Kwa hiyo, mpango huu kwa ajili mto huo tunao katika mradi wetu mkubwa.