Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 33 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 275 2019-05-22

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB N. MWAMWINDI aliuliza:-

Katika kuboresha utalii katika Hifadhi ya Ruaha:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kiwango cha lami barabara iendayo Hifadhi ya Ruaha pamoja na kuimarisha miundombinu ya ndani ya Hifadhi hiyo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Nuhu Mwamwindi Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mipango ya kukamilisha ujenzi wa barabara iendayo Hifadhi ya Taifa ya Ruaha yenye urefu wa kilomita 130 kwa kiwango cha lami. Hadi sasa, kipande cha barabara hiyo kutoka Iringa mjini hadi Kalenga chenye urefu wa kilometa 14 kimeshajengwa kwa kiwango cha lami. Sambamba na ujenzi wa barabara hiyo, pia miundombinu ya ndani ya Hifadhi ya Taifa Ruaha inaimarishwa.

Mheshimiwa Spika, jukumu la ujenzi wa barabara zilizoko nje ya hifadhi ni la Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TARURA na Wakala wa Ujenzi wa barabara TANROADS. Wizara itaendelea kufuatilia kwa karibu mamlaka zinazohusika ili kuzishawishi ziweke barabara hiyo katika Mpango Kazi wa uendelezaji wa barabra za Mkoa.

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa ina utaratibu wa kufanya ukarabati wa miundombinu ndani ya hifadhi za wanyamapori kila mwaka, pamoja na kuongeza miundombinu mipya pale inapohitajika. Hifadhi ya Taifa Ruaha, ina mtandao wa barabara za utalii zenye urefu wa takriban kilometa 1,590. Hifadhi ya Taifa Ruaha kupitia mpango wake kukuza na kuendeleza utalii Kanda ya Kusini REGROW imepanga kukarabati na kufungua barabara za utalii zenye urefu wa kilometa 1,055 katika kipindi cha miaka mitano ya mradi huo.