Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Visiwa vya Ukerewe bado havitumiki ipasavyo kama eneo mahsusi kiutalii ingawa vimo vivutio vingi vya utalii ikiwemo jiwe linalocheza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kushirikiana na vikundi kama vile vya mila na desturi Ukerewe (KUMIDEU) katika kukitangaza Kisiwa cha Ukerewe kama eneo la utalii?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya kuuliza maswali ya nyoneza. Kwanza nipongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nitakuwa na maswali mawili, la kwanza kwa mujibu wa maelezo ya waziri, Wizara inafungua Ofisi za Kanda Mwanza pale zikijumuisha Idara ya Utalii pamoja na kodi ya utalii, lakini kuna taarifa kwamba TANAPA imegawa shughuli zake Kikanda, na moja ya Kanda hizo ni Kanda ya Kaskazini Magharibi na kwa mujibu wa taarifa tulizonazo ni kwamba uongozi wa bodi umeelekeza Ofisi za Kanda ziwe Bunda eneo ambalo ni jarani sana na Serengeti. Lakini ili kusaidia ukuzaji wa utalii kwenye maeneo ya Ukerewe, Saanane, Lubondo nakadhalika. Ni kwa nini Ofisi za TANAPA za Kanda hizi, Kanda ya Kaskazini Magharibi isiwe Mwanza ziliko Ofisi za Utalii pamoja na Bodi ya Utalii badala yake zipelekwe Bunda? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kama Mheshimiwa Waziri alivyosema Wizara tayari imetambua uwepo wa vivutio vya utalii na sasa inahitaji kuviendeleza na kuvitangaza. Sasa ili kufanikisha hili ni kwa nini wizara sasa isiwekeze pesa pale Ukerewe kwa ajili ya maandalizi ya miundombinu lakini pamoja na ku-train wadau mbalimbali wakiwemo hizi local groups ambazo zimekuwa zikibainisha vivutio hivi ili kama maandalizi sasa ya kukuza na kutangaza utalii ulioko kwenye Visiwa vya Ukerewe? Nashukuru sana.(Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninamshukuru kwa pongezi zake, kwa wizara ambazo amezitoa na kulidhika na majibu yake ya maswali ya msingi. Lakini Mheshimiwa Mkundi ameomba kufahamu kwamba TANAPA katika juhudi za kuboresha shughuli za kukuza na kusimamia uhifadhi na utalii wamefungua Ofisi Kaskazini Magharibi, lakini Ofisi hiyo wameipeleka Bunda badala ya Mwanza na ameshauri kwa nini Ofisi hiyo isikae Mwanza ambapo kuna Ofisi za TTB na Ofisi za utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakubaliana na ushauri wa Mheshimiwa Mbunge nitawasiliana na TANAPA na kuona sababu za msingi zilizowapeleka Bunda, lakini ninaamini kwamba ushauri wake ni wa msingi kwa sababu Mwanza bado ni kitovu cha Kanda ya Ziwa ambapo ingelikuwa rahisi zaidi kuwahudumia wateja kuliko Bunda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wake wa pili swali langu la msingi limejibu kwamba baada ya kuziimarisha vituo hivi vyote vya mali kale tunajielekeza sasa kwenye kushirikiana na taasisi zetu mbalimbali ambazo tutazikabidhi kwenye maeneo mengi ili ziweze kuviambatanisha vituo hivi pamoja vivutio mbalimbali vya utalii kama nilivyosema Saanane na Lubondo. Kwa hiyo, nimuhakikkishie Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya vituo ambavyo tutahakikisha kwamba vinapata pesa kwa ajili ya uendelezaji na kwa ajili ya kuviimarisha itakuwa ni Ukerewe ili kuhakikisha kwamba Kisiwa cha Kirewe kinatumika kama Kisiwa cha utalii katika Ziwa Victoria.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Visiwa vya Ukerewe bado havitumiki ipasavyo kama eneo mahsusi kiutalii ingawa vimo vivutio vingi vya utalii ikiwemo jiwe linalocheza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kushirikiana na vikundi kama vile vya mila na desturi Ukerewe (KUMIDEU) katika kukitangaza Kisiwa cha Ukerewe kama eneo la utalii?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, mwaka 2014 Tanzania ilikuwa inashika nafasi ya pili kwa vivutio vya utalii kati ya nchi 133 vyenye kushindana kwenye ubora wa vivutio vya utalii duniani ambapo GDP yetu wakati huo ilikuwa ni asilimia 17 na miundombinu ya utalii ya vivutio ya kutoa ubora wa utalii ilikuwa tunashika nafasi ya 110 kati ya nchi 133.

Je, kwa mwaka huu Tanzania inashika nafasi ya ngapi kwenye ubora vivutio vya utalii duniani na tunashika nafasi ya ngapi kwenye miundombinu bora ya kuchochea vivutio bora vya utalii duniani? Ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASII NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba miaka hiyo 1984 anayosema Tanzania ilikuwa ni nchi ya pili kwa vivutio na bado ni nchi inayoongoza kwa vivutio vya utalii duniani na hivi karibuni nafikiri uliona mchakato wa kuingiza moja ya vivutio muhimu kabisa ambavyo vilikuwa vinatangazwa kwenye vivutio vya dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake kimsingi ili niweze kulijibu vizuri na kufahamu takwimu zote ambazo amezisema ni kwamba lilipaswa kuwa swali la msingi lakini nimuhakikishie Tanzania bado ni nchi yenye vivutio bora na ni nchi ambayo katika Afrika ni nchi ambayo ina vivutio bora zaidi na katika dunia ni nchi ambayo ni huwa nadhani ni nchi ya pili baada ya Brazil.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, utafiti uliofanyika kati ya mwaka 2012 mpaka 2014 ulitoa taarifa kwamba Tanzania inashika nafasi ya pili kwa vivutio vya nature duniani. Kutokea kipindi hicho mpaka sasa haujafanyika utafiti mwingine wa kuweza kutupa position yoyote ile tofauti na ile ya awali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini matokeo ya katikati ya utafiti huu ambao unafanyika kila baada ya miaka mitano yalitoka Tanzania ilionekana imeshuka kutoka nafasi ya pili mpaka nafasi ya nane kwa vivutio vya nature duniani. Na sababu kubwa iliyosababisha Tanzania kushuka ilikuwa ni uharibifu wa mazingira pia ikiwemo uvamizi wa mifugo na makazi katika maeneo ya vivutio vya utalii vya nature. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kazi kubwa imefanyika katika Awamu ya Tano ya kuwaondoa wananchi ambao wamevamia maeneo hayo, pia kupandisha hadhi baadhi ya maeneo, ninauhakika watakapofikia conclusion ya utafiti huo baada ya miaka mitano ambao ni mwaka huu pengine matokeo ya nafasi ambayo Tanzania inashika katika vivutio vya nature inaweza ikawa imeongezeka zaidi. (Makofi)