Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Katika jitihada za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za kuboresha uchumi, viongozi wa Jumuiya hiyo walipitisha utengenezaji wa Bandari ya Wete – Pemba; Je, mpango huo umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza, pamoja na majibu hayo, si ya kuridhisha kwa sababu Mheshimiwa Naibu Waziri Bunge lililopita Abdallah Mabodi alishasema kuwa pesa zimeshatengwa kwa bandari hiyo lakini mpaka sasa hivi bado yaliyofanywa ni madogo tu. Je, ni lini itajengwa bandari hiyo kwa sababu ina umuhimu sana Bandari ya Wete?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Bandari iliyoko Zanzibar ni bandari kuu, ambayo huwa wafanyabiashara wote wanaitegema bandari hiyo na bandari hiyo ni ndogo inabeba meli moja tu kuteremsha mizigo na meli hiyo inapoteremsha mizigo inachukua kati ya wiki tatu mpaka nne na kusababisha meli kuondoka na kuteremsha mizigo Bandari ya Mombasa, nchi jirani na kuikosesha mapato Serikali ya Tanzania. Je, ni lini utafanyika upanuzi wa bandari hiyo ili tuondokane na matatizo. Ahsante. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu la msingi kwamba Serikali ilitazama mahitaji kwa maana yale mahitaji ambayo nimejibu katika jibu la msingi yamefanyika, huu upanuzi ambao nimeutaja hapa lengo ni kuhakikisha kwamba wakati hizi juhudi kubwa zinafanyika za kufanya maboresho makubwa, zile huduma muhimu zinaendelea kufanyika katika bandari hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba nilikuwa najaribu kufanya rejea kwenye commitment nzima ya upanuzi wa bandari upande wa Zanzibar. Kiasi ambacho kilipitishwa na wakuu wa nchi kama level funding kwa ajili ya bandari za Zanzibar peke yake ni dola milioni 2.131. hii ni kuonesha kuwa wakuu wako committed kuonesha kwamba tunafanya maboresho makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati huo sasa utaratibu ule wa kutafuta fedha unaendelea kufanya upanuzi mkubwa ndiyo maana unaona juhudi zimefanyika na juhudi zinaendelea ili kuhakikisha tunafanya maboresho makubwa. Kwa hiyo, nikutoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba upanuzi utafanyika, hii ni commitment ya hali ya juu ambayo inasimamiwa na wakuu wa nchi, tutakwenda kufanya upanuzi wa bandari hii.

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Katika jitihada za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za kuboresha uchumi, viongozi wa Jumuiya hiyo walipitisha utengenezaji wa Bandari ya Wete – Pemba; Je, mpango huo umefikia wapi?

Supplementary Question 2

MHE. MATTAR ALI SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Bandari ya Zanzibar kiukweli kwa sasa imekuwa ndogo sana na haiwezi kufanya kazi lakini Serikali zetu zimefanya mazungumzo na Benki ya Exim ya China, mpaka leo ni kimya hakuna kinachoendelea mpaka sasa. Je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha hii bandari ya Mpigaduri inajengwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mattar kwa sababu mara nyingi nimemsikia akizungumzia sana juu ya Bandari ya Mpigaduri. Mheshimiwa Matar nikuhakikishie kwamba kweli Serikali imefanya kazi kubwa, kumekuwa na hatua mbalimbali, jitihada nyingi zimefanyika kupanua bandari na wewe unafahamu kwamba juhudi za kupanua bandari zimeanza muda mrefu tangu mwaka 2011 lakini hatua ambayo imefikia sasa hivi baada ya hiyo Benki ya Exim kuchukua hatua za kufanya funding kwa ajili ya upanuzi wa bandari hii sasa hivi draft financial agreement ilishasainiwa kwa hiyo wanafanya mapitio ya mwisho ili sasa kwenda kwenye hatua ya kwenda kwenye financing na kuanza kufanya maboresho Bandari hii ya Mpigaduri au Maruhubi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Katika jitihada za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za kuboresha uchumi, viongozi wa Jumuiya hiyo walipitisha utengenezaji wa Bandari ya Wete – Pemba; Je, mpango huo umefikia wapi?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri ni mara kadhaa Serikali imekuwa ikichukua ahadi ikisema kwamba itaweza kujenga Bandari ya Wete, hayo ni masuala ya mdomoni lakini ukija kwenye vitabu halisi, kwenye Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kimataifa kwenye Vote 34 fedha hizo haziko, mmekuwa mkidanganya mara nyingi watu wa Pemba. Mmekuwa mkisema uongo mchana kweupe bila giza. Kwenye Vote 34 ndiyo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, fedha hizo huwa haziko, hamtengi lakini mmekuwa mkisema mdomoni tu. Mtuambie hasa mna mkakati gani wa ziada muone kama fedha hizi mara hii mtazipeleka na bandari hii ya Wete mtaenda kujenga. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimualike tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tuonane uone ile document ya retreat nzima. Ninapozungumza juu ya miradi 17 ambayo kwa Afrika Mashariki ambayo inasimamiwa na wakuu wa nchi, kuna commitment ya jumla ya dola 61,000,212, ni fedha nyingi sana na ukiangalia kwa undani utaona miradi ilivyochambuliwa na hatua zinazokuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ukiiangalia hii document na hii commitment ambazo tunzisema hapa ni commitment ambazo zinachukua muda mrefu na kuna action plan. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, nikuombe tu tuonane ili kwa pamoja tuzungumze ili upate picha, na uweze pia kuisema kazi nzuri Serikali inayofanya kuhusu maendelezo ya bandari hii muhimu. Ahsante sana. (Makofi)