Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:- Je, nini Mkakati wa Serikali kuhakikisha Magereza zetu zinajitegemea kwa chakula?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na nashukuru kwa majibu japo hayajajitosheleza Kilimo cha Umwagiliaji ndiyo njia pekee ya kuhakikisha kwamba tunapata chakula cha uhakika, au mavuno kwa uhakika, lakini ukiangalia katika Magereza yote tuliyonayo nasema kwamba ni Gereza la Idete pekee ndiyo wenye Kilimo hicho cha Umwagiliaji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia hata Bajeti ya mwaka huu, ya maendeleo bado Wizara hii imeendelea kutenga shilingi Bilioni tatu kwa ajili ya Kilimo, jambo ambalo bado litaendelea na utegemezi. Je, Wizara haioni sasa kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba wanaendeleza Kilimo cha Umwagiliaji ili Magereza wetu na Mahabusu waweze kupata chakula? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa takwimu zinaonyesha kwamba mahabusu ni wengi kuliko wafungwa na kwa maana hiyo ndiyo sababu chakula hakitoshi, Je, Serikali haioni sasa kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba mahabusu hasa wale wenye kesi za madai, kwa mfano kesi ya kuiba kuku nakadhalika nakadhalika, hawakai ndani ya Magereza kwa muda mrefu na kupewa shughuli nyingine ili wale wafungwa ambao ndiyo wanapaswa kufanya kazi, kwa sababu tunajua kwamba mahabusu hawaruhusiwi kufanya kazi yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali isihakikishe kwamba wale mahabusu ambao ndiyo wengi kuliko wafungwa wanaondoka kwenye Magereza na kupata kazi nyingine za nje, ili sasa Magereza wetu au wafungwa waweze kufanya kazi na waweze kujitosheleza?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuhakikishie kwamba mawazo yake aliyoyatoa ni mawazo ya Serikali, na ndiyo maana katika Bajeti yetu ya mwaka huu tumeongeza kwa kutenga fedha hizo kwa ajili ya specifically kwenye eneo la Umwagiliaji, kwa Magereza kwa Kitengule na Isopilo, kwa hiyo siyo Idete peke yake, kuna Magereza mengine. Hata juzi juzi tu nilikwenda kwenye Gereza la Songwe na niliwasisitiza juu ya umuhimu wa kufikia malengo na tukakubaliana malengo hayo yatafikiwa kwa kuhakikisha kwamba wanatumia utaratibu wa umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hii hoja ya Umwagiliaji ni hoja ambayo ni ya msingi kama ulivyozungumza na sisi kama Serikali kupitia Jeshi la Magereza tumeiona na tunaifanyia kazi. Kuhusu suala la pili, kuhusu mahabusu ni kweli hatufurahishwi na msongamano wa mahabusu katika magereza yetu. Kama ambavyo nimejibu kwa kina wakati nikichangia bajeti hapa kwamba Serikali inafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kwamba tunapunguza idadi ya mahabusu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini moja katika jambo ambalo ni la msingi ambalo nadhani hili wananchi watusaidie pamoja na wewe Mheshimiwa Mbunge ni kuhakikisha kwamba tunajitahidi kadri inavyowezekana kupunguza kufanya makosa. Tutakapopunguza kufanya makosa basi nadhani hata idadi ya mahabusu na wafungwa itapungua wakati ambapo Serikali inaendelea na jitihada nyingine mbalimbali ikiwemo kuharakisha ksi hizi ziweze kusikilizwa haraka. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:- Je, nini Mkakati wa Serikali kuhakikisha Magereza zetu zinajitegemea kwa chakula?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa muda mrefu baadhi ya vituo vya mahabusu, mahabusu wamekuwa wakitumia ndoo kama sehemu ya kujihifadhia wanavyokuwa mle ndani kwenye hivyo vituo. Je, kutumia hivyo vindoo ni sehemu ya adhabu? Kwa sababu imekuwa si tu inadhalilisha watu bali ni kukiuka haki za binadamu.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie kwamba kwa kiwango kikubwa matumizi ya ndoo yanapungua na nina takwimu baadaYe nimpatie zinazoonesha kwmaba tumefanya jitihada za kutosha kupunguza matumizi ya ndoo kwa maana ya kuongeza ujenzi vya vyombo katika magereza yetu na kwa hakika kwa kasi hii ambayo tunaenda nayo basi miaka si mingi sana tutaondokana kabisa na tatizo hili la matumizi ya ndoo katika magereza.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:- Je, nini Mkakati wa Serikali kuhakikisha Magereza zetu zinajitegemea kwa chakula?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza. Jeshi la Magereza ni kati ya taasisi ambazo zilipewa kazi maalum ya kuzalisha mbegu na hasa mbegu za nafaka. Ni kwa nini hadi sasa Jeshi la Magereza pamoja na JKT hawafanyi kazi hiyo na tatizo la mbegu ni kubwa na Wizara ya Kilimo wamekiri kwamba jambo hili limekuwa ni zito sana kwao. Ni kwa nini Jeshi la Magereza halifanyi kazi hiyo kikamilifu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango mkakati wetu wa kujitosheleza na kilimo ambao nimezungumza kwamba tumeuandaa na tunauboresha kwa mwaka huu umegusia maeneo mengi. Nimesema kwamba katika mkakati huo kuna malengo ya kuhakikisha kwamba tuna magereza 10 ya kimkakati ya kilimo ambayo yatakuwa yanazalisha chakula cha kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika kutimiza azma hiyo tunabidi tuliwezeshe Jeshi letu la Magereza kifedha ili liweze kutimiza malengo haya na ndiyo maana tunavyozungumza tayari tuna mazungumzo na Benki ya TIB, na TID kwa ajili ya kuweza kupata fedha kwa ajili ya shughuli hizo. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba katika mkakati huo, umeangalia maeneo mengi sio tu katika maeneo ya uzalishaji lakini unapozungumzia uzalishaji pamoja na zana za vitendea kazi, upatikanaji wa matrekta na ongezeko la idadi ya wafungwa katika magereza hayo ya kimkakati lakini pia na maeneo maalum ya kuweza kuhakikisha kwamba tunazalisha mbegu kwa ajili ya uzalishaji. Na hilo tutalianza katika gereza Kitwanga kule Kigoma kwenye Mkoa ambao Mheshimiwa Nsanzugwanko anatoka ili kuweza kwenda sambamba na ile dhana ya Serikali ya kuhakikisha kwamba zao la mchikichi linachukua nafasi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wazo lake ni zuri lakini ni sehemu ya mipango ambayo tunayo na mipango hii ambayo tunadhani kwamba ni muhimu sana na imetiliwa mkazo sana na Serikali hii kwa pamoja tukishirikiana tutafanikiwa.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:- Je, nini Mkakati wa Serikali kuhakikisha Magereza zetu zinajitegemea kwa chakula?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Gereza la Kwa Mngumi lililopo Korogwe linafanya shughuli za kilimo pamoja na mabwawa ya samaki na kwa bahati nzuri Naibu Waziri umeshafika pale tukushukuru kwa kuwasaidia mashine zile za kufyatulia tofali. Je, sasa mtakuwa na mpango wa kuweza kuwasaidia kuwawezesha ili waweze kupanua yale mabwawa pamoja na kilimo kama ambavyo mnaelekeza kwamba magerea waweze kujitegemea katika uzalishaji?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwenye gereza Kwamgumi lazima nikiri na naomba Mheshimiwa Mbunge hili alifikishe kama kuna uongozi ambao binafsi ulinivutia ni uongozi wa gereza la Kwamgumi wamefanya kazi kubwa sana. Ni gereza ambalo wenyewe kwa bidii zao wameweza kukamilisha miradi ya ujenzi wa nyumba nyingi kwa muda mfupi na kukamilisha zote, sio tu kufikia kile kiwango cha lenter lakini kukamilisha nyumba zote. Ndiyo maana ahadi ambayo tulitoa ya kuwapatia zile mashine za matofali tulitimiza kwa haraka na pia tukawaahidi kwamba tutawapatia mashine hizi powertiller kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, nina uhakika kwamba najua jitihada zako za kufuatilia, uendelee kunisumbuasumbua, ahadi yetu iko pale pale na nadhani tutakapoweza kufanikisha kupata powertiller tutazipeleka kwa sababu tunaamini uongozi wa gereza hili unaweza na hii iwe mfano wa magereza mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata katika ule mradi wa samaki, nimeshazungumza na kumuelekeza CDP kuhakikisha kwamba anapeleka fedha haraka ili mradi ule wa samaki wa ufugaji uweze kuendelea. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nakubaliana na wewe kuhusiana na gereza hili, kazi nzuri ambayo inafanya na nikupongeze na wewe kwa kufuatilia na kuwa karibu na Jeshi letu la Magereza kufanikisha malengo hayo. (Makofi)