Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 32 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 266 2019-05-21

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:-

Je, nini Mkakati wa Serikali kuhakikisha Magereza zetu zinajitegemea kwa chakula?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susan Lyimo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha Jeshi la Magereza linajitosheleza kwa chakula cha wafungwa na mahabusu, Serikali imeendelea kulipatia Jeshi zana na pembejeo mbalimbali za Kilimo kupitia fedha za matumizi ya kawaida na za miradi ya maendeleo. Kwenye Bajeti ya mwaka 2018/2019 Serikali imetenga fedha kwa miradi ya maendeleo ya jumla ya shilingi Bilioni tatu kwa ajili ya ununuzi wa zana mbalimbali za Kilimo na kukamilisha miundombinu ya umwagiliaji Gereza Idete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Magereza linaendelea kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano wa mwaka 2018/2019 mpaka 2022/2023 kwa kutumia raslimali zilizopo ambapo katika msimu wa mwaka 2018/2019 Jeshi limelima jumla ya ekari 5,110 za mazao ya chakula kwa mchanganuo ufuatao; mahindi ekari 3,505, mpunga ekari 1,050 na maharage ekari 555 kwa matarajio ya kuvuna jumla ya tani 9,509.25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika Awamu ya II ya utekelezaji wa Mkakati huu, Jeshi linaendelea kukamilisha andiko la Mapinduzi ya Kilimo kwa mwaka 2019/2020 na mwaka 2023/2024 likiwa na lengo la kuondokana na utegemezi wa chakula kwa wafungwa na mahabusu kutoka Serikalini.