Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Utaratibu wa kuweka pamoja watuhumiwa wenye makosa tofauti kama vile, wizi wa kuku, mazao, mauaji, ujambazi sugu na ubakaji ni utaratibu wa kawaida katika magereza na mahabusu zetu hapa nchini, hali kadhalika kwa wafungwa wenye rika tofauti:- (a) Je, Serikali haioni kuwaweka pamoja wafungwa na watuhumiwa hao ni hali hatarishi kwa mustakabali wa maisha yao ya baadae? (b) Je, Serikali haioni inapoteza nguvu kazi ya vijana wetu kwa kuwachanganya pamoja na wale wabakaji hususan vijana wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 30?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nina maswali mawili: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kupongeza Serikali kwa jitihada kubwa za maboresho kwenye magereza na pia tumeona juhudi za Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli pale alipo tembelea Gereza na Butimba na maelekezo aliyotoa na hatua zinazochukuliwa na Serikali nzima katika kupunguza kadhia ya magereza. Kama tunavyofahamu kwamba gerezani siyo kuzuri. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka takwimu, data ya wakosaji makosa na adhabu wanazozipata wakiwa magerezani na kuziweka wazi takwimu hizi ili kuona kwamba udhibiti upo na kwamba haya makosa yanaendelea yamedhibitiwa au yanapungua?

Swali la pili, Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kufikiria kuweka wigo wa kutoa adhabu za kutumikia ndani ya jamii kwa wale ambao wanamakosa ambayo si ya kuleta dhara kwenye jamii zaidi, kuliko kuwarundika kwenye magereza kwa kuwa kufanya hivyo itaweza kupunguza mzigo mkubwa wa mkusanyiko magerezani? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yake ya kwanza ilikuwa ni ushauri ambao tunaupokea kuhusiana na takwimu kuziweka wazi. Lakini swali la pili ambalo aliuliza kimsingi jambo hilo tunalo tuna utaratibu ambao unaitwa kwa lugha ya kiingereza extramurally labor ambao utaratibu huu kwa kawaida unatumika kutoa adhabu kwa maana ya adhabu za vifungo vya nje kwa baadhi ya watuhumiwa kulingana na masharti na vigezo vilivyowekwa. Kwa hiyo, utaratibu huo tunao na tunaendelea nao. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Utaratibu wa kuweka pamoja watuhumiwa wenye makosa tofauti kama vile, wizi wa kuku, mazao, mauaji, ujambazi sugu na ubakaji ni utaratibu wa kawaida katika magereza na mahabusu zetu hapa nchini, hali kadhalika kwa wafungwa wenye rika tofauti:- (a) Je, Serikali haioni kuwaweka pamoja wafungwa na watuhumiwa hao ni hali hatarishi kwa mustakabali wa maisha yao ya baadae? (b) Je, Serikali haioni inapoteza nguvu kazi ya vijana wetu kwa kuwachanganya pamoja na wale wabakaji hususan vijana wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 30?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza:
Mheshimiwa Naibu Waziri Gereza la Babati linadaiwa na BAWASA shilingi milioni 182 bili za maji hawajawahi kulipa, maana yake wafungwa wanavyokuwa wengi na matumizi ya maji yanakuwa mengi, muda mrefu watu wa BAWASA wamedai sana hiyo bili milioni 182.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nifahamu ni lini Serikali italipa deni hili la Gereza la Babati kwa BAWASA? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima nikiri kwamba taarifa za hilo deni ndiyo nazipokea hapa, kwa hiyo ninachoweza kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kujibu maswali tutafuatilia tuweze kujua ni kwa nini deni hilo halijalipwa na ili tuweza kuangalia utaratibu wa kuweza kulipa pale ambapo tutakuwa tumepata kasma ya ulipaji wa madeni kama tunavyofanya katika magereza mengine nchini.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Utaratibu wa kuweka pamoja watuhumiwa wenye makosa tofauti kama vile, wizi wa kuku, mazao, mauaji, ujambazi sugu na ubakaji ni utaratibu wa kawaida katika magereza na mahabusu zetu hapa nchini, hali kadhalika kwa wafungwa wenye rika tofauti:- (a) Je, Serikali haioni kuwaweka pamoja wafungwa na watuhumiwa hao ni hali hatarishi kwa mustakabali wa maisha yao ya baadae? (b) Je, Serikali haioni inapoteza nguvu kazi ya vijana wetu kwa kuwachanganya pamoja na wale wabakaji hususan vijana wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 30?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali kwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba Magereza mengi nchini zina mlundikano mkubwa wa wafungwa lakini wapo wafungwa ambao wamefungwa kwa ajili ya kesi ndogo ndogo kwa mfano wizi wa kuku, kugombana na waume zao na kadhalika na wamefungwa kwa sababu ya kukosa hela ya faini. Je, kwa kuwa faini hizo ni ndogo, Serikali haioni sasa kuna haja ya wafungwa hao kuwatoa na kufanya shughuli za kijamii nje ya jamii ili waweze kufidia fedha hizo ambazo Serikali inapoteza?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie pia kwamba utaratibu huo upo tuna idara maalum chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambayo inashughulika na wanasema huduma za jamii moja kati ya jukumu lake ni kuhakikisha kwamba inazingatia aina ya wafungwa wenye sifa kama ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja ili kuweza kuwapatia kazi zingine za kufanya nje, pamoja na utaratibu mwingine ambao nimeuzungumza wakati najibu swali la msingi la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo utaratibu huo tunao.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA (K.n.y. MHE. NAJMA MURTAZA GIGA) aliuliza:- Utaratibu wa kuweka pamoja watuhumiwa wenye makosa tofauti kama vile, wizi wa kuku, mazao, mauaji, ujambazi sugu na ubakaji ni utaratibu wa kawaida katika magereza na mahabusu zetu hapa nchini, hali kadhalika kwa wafungwa wenye rika tofauti:- (a) Je, Serikali haioni kuwaweka pamoja wafungwa na watuhumiwa hao ni hali hatarishi kwa mustakabali wa maisha yao ya baadae? (b) Je, Serikali haioni inapoteza nguvu kazi ya vijana wetu kwa kuwachanganya pamoja na wale wabakaji hususan vijana wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 30?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo tu kwamba wanadhurika vijana mahabusu kwa kuona tabia za wale wafungwa wabakaji, wezi na madawa ya kulevya lakini tumeshuhudia akina mama wanakuja wajawazito wanajifungulia gerezani, kuna akina mama wanakamatwa wakiwa na watoto wanakuwa nao gerezani wanachangamana na hao watu ambao wanatabia za tofauti tofauti na tunajua kabisa kwamba mtoto mchanga kuanzia zero age mpaka five years anakuwa ndiyo muda ambao anajifunza na kuweza kuweka vitu akilini, mtoto yule anakua kwenye makuzi ya gerezani anafuata zile tabia ambazo hazina maadili kabisa.

Je, Serikali ni kwa nini sasa isitafuta mbadala kama inashindwa kuwapa dhamana hawa mahabusu wenye watoto ni kwanini isitenge sehemu kabisa ya wamama wajawazito na wamama wanaonyonyesha waweze kukaa na wale watoto mpaka watakapofikia umri wa kuweza kuwatoa gerezani, kuliko kuchangamana wanaona wale akina mama saa nyingine wako uchi, wako hivi ni tabia mbaya na haiwatendei haki hawa watoto. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto hawa wanaruhusiwa kuchukuliwa na familia zao, kwa hiyo, watu wengi ambao wanafungwa, wakinamama ambao wana watoto wanapofikia umri baada ya kuacha kunyonyesha, mara nyingi huchukuliwa na jamaa zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa wale ambao watakuwa wanaendelea kubakia magerezani aidha kwa sababu ya kukosa jamaa wa kuwaangalia nje, kuna utaratibu mzuri ambao unaandaliwa na mimi binafsi nimetembelea magereza mengi sana na ninapotembelea kwenye magereza hayo hutembelea katika maeneo ya wanawake na katika mambo ambayo tunaangalia moja ni hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahakikisha kwamba watoto wale wanapata elimu, wanaandaliwa mazingira mazuri na wanasoma katika shule za nje ya gereza. Kwa hiyo, kimsingi jambo hili tunaliangalia kwa uzito wa aina yake ili kuhakikisha kwamba watoto wale hawapati madhara ya kisaikolojia wakati wanapokuwa gerezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niendelee kutoa wito kwa wakinamama kujiepusha na kufanya vitendo vya kiharifu ili kuepusha kuwaingiza katika matatizo watoto hawa hasa wanapokuwa katika umri mdogo.