Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:- Katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 Serikali iliahidi kujenga kiwanda cha sukari katika Jimbo la Rufiji, hata hivyo ardhi iliyokusudiwa kujengwa kiwanda hicho kwa sasa amepewa mwekezaji ambaye hana nia ya kujenga kiwanda hicho:- Je, ni lini Serikali itaamua kutumia Sheria ya Ardhi Na. 113 na 114 kuichukua ardhi hiyo kutoka kwa mwekezaji na kuyapa Mashirika ya Umma ili kujenga Kiwanda cha Sukari Rufiji?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme sikuwa na hakika kwamba, swali hili lilikwenda TAMISEMI na binafsi swali hili tulilielekeza Wizara ya Ardhi kwa kutambua agizo la Mheshimiwa Rais la ujenzi wa Kiwanda cha Sukari kule maeneo yetu ya Rufiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Waziri pengine atuambie Serikali imeandaa mpango gani kwa ajili ya matumizi ya ekari 150,000 ambazo zinaandaliwa baada ya ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme la Mwalimu Nyerere?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo Mheshimiwa Mchengerwa anajenga hoja, amesema alitarajia kwamba swali hili lingejibiwa na Wizara ya Ardhi, lakini wanufaika ni vile vijiji ambavyo amevitaja ambapo sisi kama TAMISEMI tuna maslahi na vijiji vile. Katika swali lake la nyongeza anataka kujua mpango wa Serikali wa matumizi ya ekari 50,000 baada ya ujenzi wa bwawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii imekuwa makini, imekuwa ikifuata taratibu zote na kuona namna gani tufanye kulingana na wakati husika. Tutaainisha baada ya kujiridhisha kwamba eneo hilo litafaa kwa ajili ya shughuli gani na Mheshimiwa Mbunge naye atapata taarifa pamoja na wananchi wanaozunguka eneo la bwawa hilo.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuongezea kidogo katika suala hilo la kuendeleza Bonde la Mto Rufiji hekta 150,000 zilizokuwa downstream baada ya Bwawa la Mwalimu Nyerere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tayari tumeshaielekeza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na imeshaanza kuainisha na kwenda huko kufanya utafiti kuonesha namna gani tutaanza kutumia kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji baada ya bwawa lile kumalizika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge aendelee kushirikiana na Serikali yake hii na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na sasa hivi tumeweka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji mpaka ngazi ya Wilaya. Kwa hiyo, kuna Afisa wa Tume ya Umwagiliaji kwenye Wilaya ya Rufiji, Mkoa wa Pwani, Kanda ya Mashariki pamoja na Taifa. Kwa timu hiyo, tutaenda kuendeleza kilimo cha umwagiliaji ambacho ni kilimo cha uhakika.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:- Katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 Serikali iliahidi kujenga kiwanda cha sukari katika Jimbo la Rufiji, hata hivyo ardhi iliyokusudiwa kujengwa kiwanda hicho kwa sasa amepewa mwekezaji ambaye hana nia ya kujenga kiwanda hicho:- Je, ni lini Serikali itaamua kutumia Sheria ya Ardhi Na. 113 na 114 kuichukua ardhi hiyo kutoka kwa mwekezaji na kuyapa Mashirika ya Umma ili kujenga Kiwanda cha Sukari Rufiji?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya vikwazo ambavyo wanakutana navyo wawekezaji wengi hapa nchini ni urasimu na mchakato mrefu unaochukua muda mrefu wa kupata vibali vya kuwekeza katika maeneo mbalimbali; na mara nyingi Serikali imekuwa ikisema kwamba, inaendelea kuona namna gani inapunguza urasimu huo. Je, ni hatua gani imefikiwa kupunguza urasimu huu ili wawekezaji wanapokuja wasikutane na hivyo vikwazo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ambazo zimechukuliwa na Serikali ni dhahiri. Kwanza Mheshimiwa Rais kwa kuanzisha Wizara mahususi kwa ajili ya kushughulikia suala la uwekezaji kulikoni ilivyokuwa zamani, ilikuwa haijulikani hasa suala hili liko wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanzisha Wizara ambayo inashughulikia uwekezaji na maelekezo na miongozo ambayo imekuwa ikitolewa na yeye mwenyewe Mheshimiwa Rais na Viongozi wengine Wakuu wa Kitaifa kwamba, tupunguze urasimu ili tuweze kuvutia uwekezaji, naamini itatuondoa katika hali ya urasimu uliokuwepo na uwekezaji utachukua tija kwa muda mfupi zaidi.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (UWEKEZAJI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongezea majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwanza kabisa napenda tu kusema kwamba anayoyasema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, lakini pia ninachosema ni kwamba tumebadilika sana ndani ya Serikali, lakini pia katika mamlaka zetu za Serikali za Mitaa. Moja, ambalo tunalifanya hivi sasa, kwanza ni kufanya mabadiliko na mapitio ya Sera yetu ya Uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tayari kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Wizara mbalimbali na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, tunavyoongea hivi sasa tayari timu iko kazini, inafanya marekebisho ya maeneo mbalimbali ambayo yamekuwa yakionekana ni vikwazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, tunashukuru sana Wizara ya Ardhi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI yenyewe, tayari tumeshaanza kuanzisha ofisi za kusaidia wawekezaji kupitia Regional Investiment Facilitation. Tayari Arusha wako katika hatua hiyo, tayari Iringa wameshaanza na tunaendelea kufanya hivyo katika mikoa mingine. Pia tunaandaa mwongozo ili mikoa yetu na mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kuwahudumia vizuri zaidi wawekezaji wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tunaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na tunaamini vikwazo vyote na mifumo mbalimbali ya udhibiti kupitia mamlaka zetu itaondolewa.