Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 111 2019-09-13

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:-

Katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 Serikali iliahidi kujenga kiwanda cha sukari katika Jimbo la Rufiji, hata hivyo ardhi iliyokusudiwa kujengwa kiwanda hicho kwa sasa amepewa mwekezaji ambaye hana nia ya kujenga kiwanda hicho:-

Je, ni lini Serikali itaamua kutumia Sheria ya Ardhi Na. 113 na 114 kuichukua ardhi hiyo kutoka kwa mwekezaji na kuyapa Mashirika ya Umma ili kujenga Kiwanda cha Sukari Rufiji?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omar Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa Serikali iliahidi kujenga kiwanda cha sukari Wilayani Rufiji baada ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kukamilisha kazi ya kuainisha maeneo yanayofaa kwa kilimo cha miwa Wilayani Rufiji na maeneo mengine nchini. Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania, kwa maana ya TIC, ilipata mwekezaji kutoka nchi ya Mauritius, Kampuni ya Rufiji Sugar Plant na Kampuni ya Agro Forest Plantations.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Rufiji Sugar Plant inategemea kuwekeza katika Vijiji vya Tawi hekta 6,600, Nyamwange hekta 1,728 ambapo Kampuni ya Agro Forest Plantation inatarajia kuwekeza katika Vijiji vya Muhoro Magharibi hekta 5,710 Muhoro Mashariki hekta 1,529 na Vijiji vya Chumbi A, B na C hekta 1,926.77. Taratibu za kupata ardhi kwenye Serikali zote za vijiji ngazi ya wilaya ilianza mwaka 1912 na kukamilika mwaka 1916. Nyaraka zote zimewasilishwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo inaendelea na taratibu zake za kujiridhisha ili itoe hati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi iliyofanywa na mwekezaji hadi sasa ni kupima mipaka ya maeneo husika, kuchukua sampuli za udongo katika vijiji vyote na kupima kiasi cha kemikali zilizopo ardhini kwa kuzingatia masharti ya kanuni za kilimo. Aidha, taratibu za uwekezaji zitaendelea baada ya kampuni hizi kupewa hatimiliki za ardhi kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati Serikali inaendelea kukamilisha taratibu hizi.