Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Mwaka 2012 Mahakama ilitoa hukumu kuwa wakulima na wafugaji wote waondoke ndani ya Hifadhi ya Jamii ya Emborley Murtangos iliyoko Wilayani Kiteto lakini baadhi ya wananchi walipinga amri hiyo na kuendelea kufanya shughuli zao na kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji:- (a) Je, Serikali imeshughulikia kwa kiasi gani mgogoro huo uliodumu kwa miaka 8? (b) Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwadhibiti na kuwaadhibu waliokiuka amri hiyo? (b) Je, nini kauli ya Serikali juu ya matumizi ya Hifadhi hiyo ili kumaliza mgogoro huo?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nami nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na ya kina. Nachukua nafasi hii pia kuipongeza sana Serikali, hasa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais wetu, John Pombe Magufuli kwa jinsi ambavyo inashughulikia kwa ukamilifu migogoro mingi ya ardhi hapa nchini na hususan katika Mkoa wetu wa Manyara. Hapa pia nimpongeze sana Mheshimiwa RC wetu, Alexander Mnyeti na ma-DC wote wa mkoa huu kwa sababu migogoro hii sasa hivi inaenda ikipungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja tu la nyongeza. Hivi karibuni Mheshimiwa Rais wetu ametoa tamko kwamba kuhusiana na migogoro hii ya ardhi ya wananchi kuvamia maeneo mbalimbali kwa ajili ya makazi, kwa ajili ya kilimo na ufugaji yapatiwe ufumbuzi haraka ili kuleta utulivu na amani kwa wananchi katika maeneo mbalimbali:-

Je, Serikali imeweza kushughulikia kwa kiwango gani matatizo haya ya migogoro ya wananchi tukijua kwamba kule Manyara kuna mgogoro unaofukuta kule vilima vitatu kuhusiana na wananchi kukosa amani na kuvamia maeneo kwa ajili ya makazi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naomba nipokee pongezi zangu kwa niaba ya Wizara na pongezi za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge Umbulla kwa kutambua kazi kubwa inayofanyika na Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Alexander Mnyeti na Wakuu wenzake wa Wilaya, Wakurugenzi wote pamoja na Watumishi wa Serikali katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Rais kwa mapenzi na ukarimu alionao kwa Watanzania aliamua kuunda kikosi kazi cha Waheshimiwa Mawaziri wanane, wamezunguka maeneo yote yenye migogoro, Wakuu wa Mikoa wameshirikishwa, Wakuu wa Wilaya wameshirikishwa, taarifa zikakusanywa. Kazi hii imeshafanyika, sasa wameandaa ripoti wamempelekea mwenye mamlaka ili aweze kuangalia na kutoa maelekezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote wa Tanzania kwamba, Mheshimiwa Rais dhamira yake ni kuondoa migogoro kati ya wananchi na wakulima, wakulima na wafugaji, ili kazi iendelee kuwa nzuri sana. Tumpe muda alifanyie kazi, kama ambavyo alikuwa na nia njema ya ku- control migogoro hii, tuwe na amani kwamba, migogoro itaisha na wananchi wetu watafurahi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Mwaka 2012 Mahakama ilitoa hukumu kuwa wakulima na wafugaji wote waondoke ndani ya Hifadhi ya Jamii ya Emborley Murtangos iliyoko Wilayani Kiteto lakini baadhi ya wananchi walipinga amri hiyo na kuendelea kufanya shughuli zao na kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji:- (a) Je, Serikali imeshughulikia kwa kiasi gani mgogoro huo uliodumu kwa miaka 8? (b) Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwadhibiti na kuwaadhibu waliokiuka amri hiyo? (b) Je, nini kauli ya Serikali juu ya matumizi ya Hifadhi hiyo ili kumaliza mgogoro huo?

Supplementary Question 2

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika timu hiyo ya Mawaziri saba ambayo Mheshimiwa Rais aliunda, walipata pia fursa ya kutembelea Jimbo la Kigoma Kusini kwenye Kata ya Buhingu, Kijiji cha Kalilani. Tangu wamekuja kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho kuhusiana na migogoro ya ardhi, mpaka leo wananchi hawajapata majibu kuhusu hatima ya maamuzi ni kitu gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri leo hii aweze kuwaambia wananchi wa Kijiji cha Kalilani na wananchi wa Kijiji cha Sibwesa, kwa sababu wanaishi kwa mashaka hawajui watatolewa kwenye ardhi yao au wataendelea kubaki: Je, ni lini? Maamuzi ya Serikali yanasema nini kuhusiana na timu ile iliyoundwa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nimetoka kujibu swali la nyongeza hapa la Mheshimiwa Umbulla kwamba hii kazi ya kuondoa migogoro na kupanua baadhi ya maeneo ili wakulima wetu na wafugaji wapate maeneo na kupunguza migogoro, ni kazi ambayo Mheshimiwa Rais kwa ukarimu wake yeye mwenyewe aliamua kuunda timu ya Waheshimiwa Mawaziri na akawatuma, wamezunguka nchi nzima. Namaomba Mheshimiwa Mbunge na Watanzania wote, Mheshimiwa Rais ameona tatizo, amechukua hatua, mambo haya yanahitaji mambo mbalimbali ya kiutaratibu yafanyike na kila sekta ijiridhishe na kuangalia sheria mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumpe nafasi Mheshimiwa Rais nia yake njema itimie. Mgogoro huu utaisha Mheshimiwa Mbunge na wananchi wako wa Kigoma Kusini wataendelea kuwa na amani, kwa sababu Rais mwenyewe ameshika mpini na ameamua migogoro ipunguzwe. Jambo jema ni kwamba hata maeneo ambayo yalikuwa na malalamiko, ameelekeza watu wengine wasivunjiwe kuna uwezekano wa kuongeza maeneo au kupunguza maeneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamwamini Mheshimiwa Rais, ana nia njema. Jambo hili litafika mahali pazuri sana. Ahsante.