Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Usanifu na upembuzi wa kina wa mradi wa maji wa vijiji 57 Wilayani Kyerwa umekamilika muda mrefu. Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza ili wananchi wa Kyerwa waweze kupata maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwanza niipongeze Serikali kwa juhudi ambazo zinaendelea kuwapatia wananchi wa Jimbo la Kyerwa maji na napongeza kwa ajili ya mradi wa Rutunguru, Kaisho na Isingiro ambao mkandarasi alisimamishwa lakini mradi huu umeanza, naipongeza Serikali.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza Mheshimiwa Waziri alipofika Kyerwa tulikaa na kukubaliana mradi huu utakapoanza uweze kwenda kwenye Kijiji cha Kagenyi ambacho tumejenga hospitali ya wilaya, lakini kwenye vijiji ambavyo mmevieleza Kijiji cha Kagenyi hakipo. Ninaomba Mheshimiwa Waziri unihakikishie hospitali yetu ya wilaya ambayo iko kwenye Kijiji cha Kagenyi itapelekewa maji? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuna mradi unaoendelea kwenye Kata ya Mabera lakini kumekuwepo na ucheleweshwaji wa kulipwa mkandarasi na sasa hivi anadai zaidi ya milioni 150. Mheshimiwa Waziri ni lini mkandarasi huyo atalipwa ili mradi huu uweze kukamilika na wananchi wa Kata ya Mabera waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kiukweli naomba nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge ni miongoni mwa Wabunge ambao ni wachapakazi na ni wapiganaji hususan maendeleo ya wananchi wake. Kikubwa binafsi nimekwenda na Mheshimiwa Waziri amekwenda kuhusu suala la huu utekelezaji wa mradi huu mkubwa.

Mheshimiwa Spika, sasa nachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kutokana na jitihada kubwa ambazo amezifanya ujenzi wa hospitali ile kubwa sisi kama Wizara ya Maji hatutokuwa kikwazo, namhakikishia kijiji kile tutakipelekea huduma hii ya maji.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu swali lake la pili tuna mrai ambao tunautekeleza katika Kata ya Mabira, mradi takribani milioni 586, upo asilimia 80 ambao unatekelezwa na mkandarasi ambaye anaitwa Vumwe Company Ltd anadai takribani milioni 137. Nataka nimhakikishie ndani ya mwezi huu tutalipa fedha ile ili mradi ukamilike na wananchi waweze kupata huduma ya maji na mimi nipo tayari kwenda kuufungua kuambatana na Mheshimiwa Mbunge.

Name

Stephen Julius Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Primary Question

INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Usanifu na upembuzi wa kina wa mradi wa maji wa vijiji 57 Wilayani Kyerwa umekamilika muda mrefu. Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza ili wananchi wa Kyerwa waweze kupata maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa mradi wa KASHUWASA wa kutoa maji Ziwa Victoria kuleta katika Mji wa Shinyanga na Kahama. Katika mradi ule vijiji vyote vinavyopitia pembezoni mwa bomba hilo vilipaswa kuunganishwa na maji ya Ziwa Victoria. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri alipofanya ziara na Mheshimiwa Makamu wa Rais alituahidi kutupatia pesa katika vijiji vya Bugwandege, Kata ya Ibadakuli, vijiji vya Mwanubi Kata ya Kolandoto, Chibe katika Kijiji cha Mwakalala pamoja na Kijiji cha Ihapa ambapo tank kubwa la Kashuwasa limejengwa pale lakini wananchi wale hawajapatiwa maji.

Swali langu ni kwamba, sasa ni lini zile pesa alizoahidi zitakuja na ili wananchi wale waweze kupatiwa maji kama alivyoahidi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Masele kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. Kiukweli kama Serikali tunatambua Mkoa wa shinyanga ni moja ya maeneo yalikuwa na changamoto kubwa sana ya maji na Serikali ikawekeza fedha kwa ajili ya kuyatoa maji Ziwa Victoria na kuyapeleka katika Mji wa Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kweli vipo baadhi ya vijiji ambavyo havina maji na jukumu la kuwapatia maji ni jukumu letu sisi Wizara ya Maji. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge tukutane sasa haraka na wataalam wetu ili tuangalie namna ya kuweza kutekeleza ahadi hiyo ambayo tuliahidi, ahsante sana.