Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 107 2019-09-12

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Usanifu na upembuzi wa kina wa mradi wa maji wa vijiji 57 Wilayani Kyerwa umekamilika muda mrefu. Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo utaanza ili wananchi wa Kyerwa waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako naomba nitoe pole kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga kwa kuondokewa na kipenzi chetu aliyekuwa Mbunge Mheshimiwa Omary Nundu Mwenyezi Mungu ailaze mahala pema roho yake peponi.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wialya ya Kyerwa ni mojawapo ya wilaya zinazounda Mkoa wa Kagera na kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji imefika asilimia 45.6 kutokana na asilimia ya upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kuwa Serikali iliamua kubuni mradi mkubwa utakaoweza kuhudumia wananchi zaidi ya 232,000 walioko kwenye vijiji 57 kutoka kwenye chanzo kimoja ambacho ni Ziwa Rushwa kando na Mto Kagera. Kazi hii alipewa mtaalam mshauri Don Consult na aliweza kukamilisha kazi hiyo mwaka 2018.

Mheshimiwa Spika, taarifa ya usanifu pamoja na makisio ua utekelezaji wa mradi huo ni shilingi bilioni 144.

Baada ya kupitia gharama hizo, Serikali imeamua kupitia upya usanifu huo ili kujiridhisha na mfumo wa ujenzi uliopendekezwa na gharama za ujenzi wa mradi huo. Serikali imeamua kuchukua hatua na uamuzi huo kutokana na uzoefu ulipatikana kuwa baadhi ya miradi mikubwa imekuwa na gharama kubwa bila kuzingatia uhalisia wa teknolojia inayopendekezwa na pia uwezo wa uendeshaji wa jamii husika.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo wakati taratibu hizo zinaendelea, Serikali kwa upande wake inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo kwa kadri mapitio ya usanifu yatakavyoonesha na utatekelezwa kwa awamu. Kwa kuanza, mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga shilingi bilioni moja zitakazoanza kutekeleza mradi huo kwa awamu kwenye vijiji vya Mkiyonza, Nshunga, Milambi, Mkombozi, Rukuraijo, Nyabikurungo na Nyaruzumbura. Hivyo, Serikali inamuomba Mheshimiwa Mbunge kuwa mvumilivu wakati Serikali inaendelea kukamilisha mapitio ya usanifu kwa lengo la kuanza kutekeleza mradi huo.